Na John Walter -Manyara
Naibu
waziri wa Nishati mheshimiwa Stephen Byabato ameliagiza shirika la Umeme
nchini (TANESCO) mkoani Manyara kuwaunganishia Umeme wananchi wote
Waliolipia gharama zinazohitajika kabla ya mwezi Agosti kuisha.
Ametoa
agizo hilo wakati akizungumza na Wananchi katika Kata ya Tumati kijiji
cha Mongahay wilayani Mbulu Kwenye hafla ya kuzindua na kuwashwa Umeme
katika eneo hilo ikiwa ni mradi wa usambazaji wa Umeme vijijini (REA)
awamu ya tatu mzunguko wa pili.
Amesema serikali haitomvumilia mkandarasi au kiongozi wa Tanesco atakaekwamisha shughuli ya kuwapatia wananchi nishati ya Umeme.
Amesema
agizo la serikali gharama za Umeme mkubwa ni shilingi 139,500 na Umeme
mdogo ni shilingi 27,000 na atakaekiuka atachukuliwa hatua stahiki.
Katika hatua nyingine amewataka viongozi kuendelea kuwasisitiza wananchi kujitokeza kulipia gharama hizo ili kupatiwa huduma.
Mkuu
wa wilaya ya Mbulu Sezaria Makotha amesema Vijiji 48 vya wilaya hiyo
Kati ya Vijiji 110 vimeshapata Umeme ikiwa ni jitihada za ufuatiliaji wa
karibu wa meneja wa Tanesco Mbulu Mhandisi Faustina Tuyaa.
Aidha
Vijiji 71 vilivyobaki katika wilaya ya Mbulu vimeingizwa katika mpango
wa awamu hii ili kutimiza adhma ya serikali ya kufikisha Umeme katika
vijiji pamoja na vitongoji vyote nchini ifikapo mwaka 2022.
Mbunge
wa Mbulu vijijini Flatey Massay ameishukuru serikali kwa kuendelea
kuwasogezea wananchi huduma hiyo ambayo itawawezesha kufanya shughuli
mbalimbali za uzalishaji huku akiomba tatizo la mita za luku lifanyiwe
Kazi na bili iwe tofauti na mjini.
Meneja
wa Tanesco wilayani humo Faustina Tuyaa ameahidi kusimamia kikamilifu
wakandarasi wanaotekeleza mradi huo ili ukamilike kwa wakati
uliokusudiwa.
No comments:
Post a Comment