Waziri wa Maliasili na Utalii,
Dkt.Damas Ndumbaro amewataka Watumishi wote wanaofanya kazi katika
Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii wajiandae
kisaikolojia kupitia mfumo wa mafunzo ya Kijeshi.
Ametoa agizo
hilo mwishoni mwa wiki wakati alipokuwa akizungumza na Watumishi wa
Chuo cha Misitu Olmotonyi kilichopo Jijini Arusha ikiwa ni ziara ya
kikazi Chuoni hapo ya kuwatembelea na kuzungumza na Watumishi hao ili
kujua changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi
Amesema
mabadiliko ya mfumo wa utendaji kutoka ule wa kiraia kwenda katika mfumo
wa Jeshi Usu, yanalenga kuleta suluhisho la kudumu katika kukabiliana
na changamoto za usimamizi wa rasilimali misitu na nyuki pamoja na
wanyamapori nchini.
Amesema hakuna Mtumishi yeyote wa Taasisi
hizo atakayekwepa mafunzo hayo kwa vile hiyo ni sera ya Wizara huku
akisisitiza kuwa hilo halikwepeki na yeyote ambaye hayupo tayari basi
ahame wizara hiyo ndiyo itakuwa salimika yake
" Leo unaweza
kuhamishwa kutoka Olmotonyi kwenda Shirika la Hifadhi za Taifa ( TANAPA)
au TFS wenzako kule washakamilika tayari ni wanajeshi, wewe utakuwa
raia" alihoji Dkt.Ndumbaro
Amesisitiza kuwa kila mtumishi
aliyeko katika Taasisi hizo lazima apitie mafunzo hayo kwa sababu
watakuwa wakihamishwa kutoka Taasisi moja hadi nyingine ndani ya Wizara
hivyo endapo hajapitia mafunzo hayo itamuwia vigumu katika kutekeleza
majukumu yao wakati akiwa raia katika mfumo wa kijeshi.
Amezitaja
Taasisi hizo kuwa ni Mfuko wa Misitu Tanzania (TFF) Mfuko wa
Wanyamapori Tanzania ( TWPF) Bodi ya Utalii Tanzania ( TTB) Chuo cha
Taifa cha Utalii ( NCT) Chuo cha Misitu Olmotonyi, Chuo cha Usimamizi wa
Wanyamapori Mweka, Chuo cha Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi,
Makumbusho ya Taifa (NMT), ChUo cha Nyuki Tabora (BTI), Taasisi ya
Utafiti ya Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) Taasisi ya Utafirti wa Misitu
(TAFORI) TAWA, TANAPA na TFS
Kupitia agizo hilo,Dkt.Ndumbaro
amezitaka Taasisi hizo kujiandaa kushiriki katika mafunzo hayo ambapo
amesema mafunzo hayo yatatolewa kwa awamu awamu.
Akizungumza na
Watumishi hao wa Chuo cha Olmotonyi, Dkt.Ndumbaro amesema anataka
wanavyowafundisha wanafunzi wao ambao wataajiriwa TFS inayoendeshwa
kijeshi ni lazima wakufunzi wao wawe wanajeshi kwanza
"
Haiwezekani mnawafundisha Wanafunzi waende kuajiriwa huko TFS kama
wanajeshi wakati ninyi sio wanajeshi, mnawafundisha nini " alihoji
Ndumbaro
Awali, Kamishna Uhifadhi wa TFS, Prof.Dos Santos Silayo
alieleza kuwa kwa vile TFS ndo imekuwa muajiri mkuu wa Wahitimu wa Chuo
hicho hivyo wameanza utaratibu wa kuhakikisha baadhi ya kozi katika Chuo
hicho ziwe na mafunzo ya kijeshi ili kuwaandaa wanafunzi wa Chuo hicho
wanapoajiriwa na TFS
Alisema ili kuhakikisha hilo linafanikiwa
wao kama TFS imekichagua Chuo hicho kuwa mojawapo ya kituo cha Mafunzo
ya kijeshi kwa baadhi ya Maafisa kutoka TFS.
No comments:
Post a Comment