HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 12, 2021

Mgomo wa wakulima uliodumu kwa mwezi mmoja wasitishwa, warejea shambani kwa masharti

 

Na Amiri Kilagalila,Njombe

Muungano wa wakulima wa zao la chai kupitia vyama vya ushirika MVYULU tarafa ya Lupembe mkoani Njombe wamekubaliana kusitisha mgomo wa uchumaji wa majani ya chai uliodumu kwa mwezi mmoja na kukubaliana kurejea shambani hapo kesho April 12 mara baada ya makubaliano ya ulipwaji wa madeni yao zaidi ya Bil 1 kutoka kwa wawekezaji wa viwanda vya Ikanga na Igombola.

Mbunge wa jimbo la Lupembe Edwin Swale amesema uamuzi huo umefikia mara baada ya majadiliano kadhaa ikiwamo vikao vya mara kwa mara yaliokuwa yakifanywa baina ya serikali,wakulima,uongozi wa vyama vya ushirika pamoja na wawekezaji wa viwanda hivyo vya Ikanga na kiwanda cha Chai Lupembe (Igombola)

“Tumefanya uamuzi huo mkubwa tukiwa tumekubaliana kwamba kuanzia sasa hatutasubiri wakulima kukaa zaidi ya miezi miwili bila kulipwa tena,kwa hiyo kwenye ahadi na wawekezaji wa Ikanga fedha ambazo wameahida kuwalipa wakulima wa chai mpaka mwishoni mwa mwezi 4, basi tarehe 15 mwezi wa 5 tunakutana kuthibitisha”alisema Edwin Swale

Amesema mgomo wa kuchuma chai ulianza March mbili kutokana na malalamiko ya wakulima hao kuto kulipwa stahiki zao ili waweze kujikimu katika maisha

“Tulifanya uamuzi huo tarehe mbili mwezi wa tatu kwamba wananchi wa tarafa ya Lupembe,tusitishe kuchuma chai na tuzungumze kwanza kuhusu malipo,wakati tunafanya uamuzi ule tulikuwa na madai ya miezi mitano ya kulipwa,na mpaka hivi ninavyozungumza mwekezaji wa Ikanga amelipa fedha ya miezi 5 na anadaiwa mwezi wa pili tu” aliongeza Edwin Swale Mbunge wa Lupembe

Ameahidi kuzungumza na waewekezaji ili kuweka utaratibu mzuri wa ulipwaji wa fedha za wakulima“Tunataka tuweke utaratibu mzuri ni lazima wakulima wa chai walipwe kila mwishoni mwa mwezi fedha yao wanayostahili kulipwa na niwahakikishie wananchi hii ndio kazi mliyonituma,niwahakikishie madai ya mwezi wa pili yatalipwa na madai ya mwaka 2018 yatalipwa” Edwin Swale Mbunge wa Lupembe akiwa kwenye mkutano na wananchi wa Lupembe

Vile vile amesema wawekezaji wa kiwanda cha Igombola mpaka sasa ndio waliobakiwa na madai ya muda mrefu ukilinganisha na madai yaliyopo kwa wawekezaji wengine kutokana na kupunguza madeni yao.

“Wawekezaji wa Igombola hali yao ni mbaya zaidi,kwasababu kuanzia mwezi wa 12,1,2 na 3 hawajawalipa fedha wakulima wa chai na ahadi waliyoitoa kwenye kikao mpaka tarehe 26 mwezi huu watakuwa wamewalipa wakulima malipo yote” Edwin Swale

Hata hivyo amewataka wakulima wa chai kuto kukata tama na kilimo hicho na kuhamia katika kilimo kingine badala yake waweze kujihusisha na kilimo kingine pia ili kuwa na uwanja mpana wa kukuza vipato vyao

“Mlio kata tamaa ya kuchuma chai na kuamua kwenda kupanda parachichi na miti,nawaombeni mfanye mambo yote,kwasabbu unavyopanda parachichi na zenyewe zikawa nyingi,kuna siku soko litaanguka kwa hiyo msitupe chai.Wajibu wangu na viongozi wengine tutahakikisha wakulima mnalipwa kwa wakati” alisema Swale

Kutokana na hali hiyo wamiliki wa viwanda hivyo wamesema kutokana na kufikia makubaliano hayo pia ikiwemo kuchuma majani safi na yenye viwango stahiki wapo tayari kukamilisha malipo kabla ya mwezi Mei huku wakulima wakikubaliana kukutana Mei 15 ili kujadili utekelezaji wa makubaliano hayo.

Mbunge wa jimbo la Lupembe Edwin Swale akiwaeleza wananchi wa Lupembe katika mkutano uliofanyika eneo la Barazani namna walivyofanya vikao vya mara kwa mara na kufikia makubaliano mazuri na wawekezaji kuwalipa wakulima kwa wakati stahiki zao.
Baadhi ya wakulima na wananchi wa jimbo la Lupembe wilayani Njombe wakati wakimsikiliza mbunge wao mikakati sahihi ya upataji wa stahiki zao mara baada ya kufikisha majani ya chai viwandani.
Mfano wa Shamba la chai na wakulima wakionekana katika shughuli yao ya kusafisha shamba ili kuboresha mashamba hayo,picha ni kutoka mtandaoni.



 



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad