NA FARIDA SAIDY, MOROGORO.
Vijana
wametakiwa kuzingatia tabia chanya za usafi katika maeneo hayo ikiwemo
kunawa mikono,kutumia maji safi pamoja na kudhibiti kusambaa kwa taka
ngumu katika maeneo yao hali itakayosaidia kutunza na kulinda mazingira.
Wito
huo umetolewa wakati wa kampeni ya KIJANA NI USAFI ambayo inalenga
kuhamasisha tabia ya usafi kwa vijana wakitanzania inayosimamiwa na
Shirika la Raleigh Tanzania chini ya ufadhili wa shirika la msaada wa
Uingereza( UKAID).
Kampeni hiyo itakayodumu ndani
ya miezi 6 inawalenga vijana wa wakike na kiume wenye umri wa miaka kati
ya 15-35,ambapo inatarajia kufikia zaidi ya vijana 48,000 katika mikoa
ya minne ambayo ni Iringa,Morogoro,Dodoma na Dar es salaam.
Akizungumza
katika kampeni hiyo Mratibu wa Mradi,Bwana Augustino Dickson amesema
kampeni hiyo katika Manispaa ya Morogoro itajikita katika itahimiza
matumizi ya maji safi na salama,na kuitaka jamii kuacha kuishi kwa
mazoea.
Hata hivyo ameongeza kuwa Mkoa wa Morogoro
unaathiwa na Magonjwa ya mlipuko ya mara kwa mara ya kiwemo mlipuko wa
ugonjwa wa Kipindupindu hali ambayo inatokana na jamii kutotumia maji
safi na salama.
Aidha ameongeza kuwa kampeni ya
KIJANA NI USAFI itaendelea kulenga kundi la vijana kwa sababu vijana
ndio kundi lenye idadi kubwa ya watu Nchini, huku akiongeza kuwa vijana
wanaweza kuwa wakala wa mabadiliko chanya katika jamii endepo
watajengewa uwezo kuhusu elimu ya mazingiara.
Katika
kampeni mafunzo mbalimbalia ya namna ya kuhifadhi maji safi na salama
yametolewa kwa wananchi,huku wakazi wa Manispaa ya Morogoro
wakilishukuru Shirika la Raleigh Tanzania kwa kuwapatia elimu ya
mazingira.
No comments:
Post a Comment