HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 30, 2019

MEJA KUNTA AWAOMBA WASANII WA SINGELI KUUMIZA KICHWA KUTUNGA NYIMBO ZENYE KUJENGA JAMII

Na Khadija Seif, Michuzi TV

MSANII chipukizi wa Muziki wa Singeli Mwalami sadiki(Meja kunta) amewataka wadau wa Muziki kutoa ushirikiano na kuuchukulia o muziki wa Singeli wa kipekee sana.

Meja amesema ni wakati umefika tuwaaminishe kuwa tunaweza na tutaufikisha mziki wa Singeli mbali kwa ni wakipekee na unapatikana Tanzania tu.

Pia ametoa ushauri kwa waimbaji wasingeli kujaribu kujichanganya na kufanya kazi na wasanii wa miziki mbalimbali kama taarabu,bolingo, Bongofleva.

"Tusijitenge sana, tujichanganye na ndio maana Nina ndoto za kufanya kazi na Vanessa mdee,"Aidha amesema bado amekumbana na changamoto nyingi sana tangu aingie rasmi kwenye fani hiyo ya muziki wa Singeli.

"Bado kuna baadhi ya jamii wanaamini Muziki wa Singeli ni wakihuni haufai katika jamii kutokana na baadhi ya tungo nyingi kuhamasisha mambo ya kihuni,"

Hata hivyo amewashukuru mshabiki zake kumpokea vizuri kwenye Muziki huo wa Singeli na kibao chake cha "Mamu" kuendelea kutikisa kila kona.

"Bado naendelea kuumiza kichwa ili kuendelea kuwa pamoja na mashabiki zangu na nimelenga hasa kwenye tungo zenye kutufundisha na kutujenga zaidi kuliko kupotosha jamii yetu,"Nina ndoto za kufanya kazi na msau,"

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad