HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 30, 2019

MAHAKAMA YA TANZANIA YATOA ELIMU KUHUSU MAHAKAMA INAYOTEMBEA DAR



Wakazi wa Boko jijini Dar es Salaam wakisoma vipeperushi vya Mahakama inayotembea wakati gari maalum la Mahakama hiyo lilipokuwa likitoa elimu kwa umma  kuhusu Mahakama hiyo.
 Dereva wa pikipiki akisoma kipeperushi cha gari  maalum la  Mahakama inayotembea leo wakati wa utoaji elimu kwa umma kuhusu mahakama hiyo, huku wenzake wakiendelea kusikiliza matangazo yaliyokuwa yakitolewa  na gari hilo kwenye eneo la Boko Magengeni, jijini Dar es Salaam 
 Wananchi wakipatiwa elimu kuhusu Mahakama inayotembea na Karani Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Nise Mwasalemba ndani ya gari hilo maalum lililokuwa limepaki eneo la Ofisi ya Mtendaji Kata ya Bunju.
Karani wa Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Nise Mwasalemba(mwenye shati la njano ndani ya gari hilo maalum ) akitoa elimu  kwa umma kuhusu Mahakama inayotembea na shughuli zitakazofanywa na Mahakama hiyo, kwa wakazi wa Boko Magengeni, jijini Dar es Salaam wakati wa utoaji wa elimu kwa Umma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad