Assalaam Aleikum.
Salaam zangu za Mei Mosi
Kwanza sote tumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma anaendelea kutupa uhai na uzima hadi siku ya leo.
Hakika pumzi hii ndio inatufanya
tufurahi na kuhuzunika pamoja,pia ndio inayotufanya tuweze kuandika na
kusoma maandiko mbalimbali ikiwemo andishi hili dogo
Jana pale uwanja wa taifa palifanyika
mechi kubwa kabisa ktk ukanda huu wa Afrika Mashariki. Simba na Yanga
zote za hapa jijini Dar.
Sio vyema kurejea kuwapa matokeo ila
Alhamdulillah klabu yangu ya Simba imefanikiwa kushinda na kujisogeza
karibu kabisa na ubingwa wa ligi kuu nchini
Nimeandika kujisogeza kwa kuwa bado
hatujatwaa ubingwa.kwa sasa tunahitaji points tano tu ili tuweze
kutawazwa ubingwa huu unaosubiriwa kwa hama na washabiki wote kote
nchini
Kiukweli hzi points tunazohitaji
tutazisaka kwa tahadhari zote na kwa kutambua kiu ya wanasimba..
tutaingia kwenye michezo ilobaki kwa nguvu kubwa na kwa umakini wa hali
ya juu,sambamba na kuwaheshimu wapinzani wetu
Ukiachana na hayo nna vitu vwili very special nataka kuvisema hapa
Kwanza ni shukran kwa washabiki wetu..ktk maisha yangu yote nilioishi sijapata kuona washabiki kama wa Simba..
Ni watu wasikivu mno na wenye subira na
upendo wa hali ya juu,ni watu wanaopenda futboll halaf ndio timu
yao,wana ustaarabu uliopitiliza na wenye mapenzi yasio na shaka kwa
klabu yao,
Kwenye ustaarabu huwa natolea mfano wa
kitendo cha kutoa back pass kwa mchezaji Hassan kesi wakati akiichezea
Simba kwa Donald Ngoma wa Yanga na kutufunga goli la kizembe zaid ktk
historia ya derby hii
Inawezeka kabisa ilikuwa ni bahati
mbaya,ila kilichostaajibisha muda mchache ujao mchezaji huyo alihamia
Yanga tena kwa maneno mabaya ya dharau na kebehi..naapa Wallah kitendo
kile ingekuwa kwa wenzetu kessi angeuhama mji huu na kurudi Morogoro
(tamka Mrogoro)
Ustaarabu wa watu wa Simba
unadhihirishwa na uvumilivu wao ktk miaka minne ya nyuma kwa vitendo
lukuli dhidi ya klabu vilivyokuwa vikifanywa na baadhi ya viongozi wa
mamlaka za Soka,na hili c vema kulirejea kutokana na sababu za
kibinadaam zaidi.
Hawa kwangu ni watu special ni watu
ambao wamenirahisishia kazi yangu ya upashaji habari..washabiki hawa ni
zaidi ya ndugu zangu ingawa wengi siwajui kwa majina na sura.
Na mfano hai ni mechi ya jana..ktk
historia ya hz timu mbili haijapata kutokea washabiki kwenda uwanjani
wengine wawe zaidi ya asilimia themanini.
Yes jana imewezekana.nimewahamasisha
wakahamasika nimewaaminisha wakaamini nimewaambia nyie ndio timu
kubwa,bora na yenye fans wengi kupita zote nchini na jana
wamelidhihirisha hilo kwa vitendo.
Hakika kama kuna tuzo ya washabiki bora nchini wanastahili kupewa Simba Sports Club.
Na kwa kupitia makala hii niwashukuru sana washabiki wetu mmetuvika nguo na sisi hatutawaangusha msimu huu,mtapata mtakacho Inshaallah
Jambo la pili nnalotaka kuandika ni
kitendo cha beki na nahodha wa Yanga kelvin Yondan kumtemea mate
mchezaji wetu Asante kwasi bila sababu yoyote na kama Tv yetu bora
nchini Azam Tv ilivyootuonyesha jana
Mara baada ya kumalizika kwa mechi ya
jana kila mshabiki aliyepata fursa ya kuongea na mm alilalamikia
'ushenzi 'ule.wapo walionipigia cm na wapo waliondika kwenye page yangu
ya Instagram..ila niliumia zaid kuona hata kwasi mwenyew akimlalamikia
meneja wetu kwa msg aliyotutumia jana usiku na kututaka management ya
klabu ilichukulie kwa uzito mkubwa jambo hili
Yondan ni mchezaji mwandamizi nchini ni
nahodha na kiongozi ndani ya uwanja na amecheza derby nyingi kupita
wachezaji wote waliocheza jana,na haitegemewi mchezaji wa calibre yake
kufanya uhuni wa aina ile.
Kumtemea mate mwanadamu mwenzio ni tusi
kwa utamaduni wa taifa lolote lile duniani.ni dharau na ni ubaguzi
ukizingatia aliyemfanyia ni raia wa Ghana.
Ni ushamba na fedheha kwa klabu yake na nchi kwa ujumla
Ni ulimbukeni na kujiona yy hawezi kufanywa lolote na mamlaka na kiukweli ni jinai pia inayofanyika ndani ya uwanja
Kwangu mm hiki ni kitendo cha hovyo
kuwahi kukishuhudia ktk derby ya Simba na Yanga...tambua mm nimehudhuria
zaidi ya derby 70 za miamba hii...
Sijapata kuona wala kusikia unyama wa aina ile uwanjani
Matarajio yetu kama klabu ni kuona hatua stahiki za kinidhamu zinachukuliwa dhidi yake tena kwa uharaka
Na kwenye hili hatutarajii kuona adhabu
nyepesi za kufungiwa mechi mbili tatu..lazma itolewe adhabu kubwa
itakayotoa fundisho kwa wachezaji wengine ili wasithubutu kufanya
uharamia kama ule
Ikumbukwe adhabu ya Juma Nyoso iliotokana na udhalilishaji..
Hatuwapangii bodi na tff lakini pia
hatutegemei huruma au kuangalia ukubwa wa timu na ktk hili hatutaandika
barua tukiamini bodi na tff wana watu makini na watenda haki
watakaoalichukulia jambo hili kwa uzito unaostahili.
Mwisho
Niwaambie tumejiandaa kisaikolojia kuwa
mabingwa ila tusifanye sherehe yoyote kwa sasa..pia tunapiga marufuku
kutengeneza jezi za Simba bingwa hadi pale tutakapofikisha points ambazo
wengine wanaziona kwetu tu
Adiooooos
Haji Manara
No comments:
Post a Comment