Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema licha ya hali
ya uchumi kushuka wakati anaingia madarakani kutokana na janga la UVIKO 19
kuathiri uchumi wa dunia, uchumi wa Tanzania kwa sasa unaimarika.
Mhe. Rais Samia amesema hayo wakati akijibu
swali katika Mdahalo wa Wakuu wa Nchi uliojadili fursa zilizomo na
changamoto zinazozikabili Nchi za Afrika uliofanyika
Accra, Ghana katika Mkutano wa 57 wa Benki ya Maendeleo ya Afrika
(AfDB).
Aidha, Mhe. Rais Samia amesema wakati wa janga la UVIKO 19
uchumi wa nchi
ulishuka kutoka asilimia 6.4
hadi asilimia 4 lakini kwa sasa umekuwa na
kufikia asilimia 5.2 kwa mwaka huu huku matarajio ni kufikia asilimia 6.7 mwaka
2025.
Vile vile, Rais Samia
amesema AfDB na Mashirika ya Kimataifa yamechangia kuendeleza kilimo, miundombinu
ya barabara pamoja na viwanja vya ndege, hivyo kusaidia kuunganisha Tanzania na
nchi jirani.
Rais Samia pia amesema kutokana
na janga la UVIKO 19, Shirika la Fedha Duniani (IMF) liliipatia Tanzania Mkopo wa
kukabiliana na janga hilo ambapo Tanzania ilitumia fedha hizo katika sekta ya
Elimu, maji pamoja na afya.
Aidha, Rais Samia amesema fedha za UVIKO 19 zimesaidia
kusambaza maji katika maeneo ya mijini na vijijini ambapo hadi kufikia mwaka 2025
anatarajia usambazaji wa maji maeneo ya vijijini kuwa asilimia 85 na asilimia
95 kwa maeneo ya mijini.
Rais
Samia Suluhu Hassan, akiwa amesimama na Rais wa Ghana Mhe. Nana
Akufo-Addo, Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi, pamoja na Rais wa Benki
ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinumwi Adesina wakati wa nyimbo za
Taifa zikipigwa kabla ya kuanza kwa Mkutano wa 57 wa AfDB unafanyika
katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Accra nchini Ghana tarehe 24
Mei, 2022.
Rais
Samia Suluhu Hassan, akizungumza katika Mdahalo pamoja na baadhi ya
Viongozi Wakuu wa nchi nyingine kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Benki ya
Maendeleo ya Afrika AfDB kujadili fursa mbalimbali pamoja na changamoto
zinazolikabili Bara la Afrika. Mkutano huo wa 57 wa AfDB unafanyika
katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Accra nchini Ghana tarehe 24
Mei, 2022.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa
katika Mkutano wa 57 wa AfDB unaofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa
Mikutano wa Accra nchini Ghana tarehe 24 Mei, 2022.
Viongozi
mbalimbali wakiwa kwenye Mkutano wa 57 wa AfDB unaofanyika katika
ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Accra nchini Ghana tarehe 24 Mei,
2022.
Mhe.
Rais Samia Suluhu Hassan, akiwa amesimama na Rais wa Ghana Mhe. Nana
Akufo-Addo, Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi, Rais wa Benki ya
Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinumwi Adesina pamoja viongozi
mbalimbali katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa
57 wa AfDB unaofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Accra
nchini Ghana tarehe 24 Mei, 2022.
No comments:
Post a Comment