Janeth Raphael - MichuziTv Dodoma
Ikiwa leo ni maadhimisho ya siku ya usikivu duniani
Wananchi
zaidi ya 126 walijitokeza kufanyiwa uchunguzi wa matatizo ya usikivu na
afya ya Masikio katika kambi maalumu ya uchunguzi inayoendelea katika
Hospitali ya Benjamini Mkapa Dodoma.
Kambi hiyo ya siku tatu
inayofanyika kuanzia tarehe 01-03 Machi, inaendeshwa na Madaktari Bingwa
wa Masikio, Pua na Koo kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (Upanga
& Mloganzila), Hospitali ya Benjamini Mkapa, KCMC, Bugando,
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na Hospitali ya Mkoa ya Dodoma.
Akizungumzia
mwenendo wa kambi hiyo, Dkt. Costantine Kaniki kutoka Hospitali ya
Mkoa wa Dodoma amesema kati ya wagonjwa 126 waliojitokeza 55
walilalamika kuwa na usikivu hafifu lakini baada ya uchunguzi 31 sawa na
asilimia 56 ndio waliobainika kuwa kweli wana tatizo na kati yao
wanawake ni 18 na wanaume ni 13.
“Miongoni mwa hao waliofanyiwa
uchunguzi wawili walibainika kupoteza usikivu kabisa ambao kiumri mmoja
ana miaka 69 wakati mwingine ana miaka 22” amesema Dkt. Kaniki.
Akizungumzia
sababu mbalimbali zinapelekea mtu kupoteza usikivu Dkt. Godlove Mfuko
kutoka Muhimbili Mloganzila amesema kuwa zipo sababu nyingi ikiwemo
mtoto kuzaliwa njiti na athari za dawa lakini kelele inatajwa kuwa ndio
sababu kubwa inayopelekea watu wengi kupoteza usijivu duniani.
“Sauti
kubwa inaharibu masikio na kupelea usikivu hafifu kwa kuwa sauti kubwa
inaharibu seli za usikivu na hupelekea mtu kusikia milio isiyo ya
kawaida au kupoteza usikivu.
Amesema kwamba watu wanaofanya kazi
au wenye mazoea ya kutembelea kwenye maeneo yenye kelele nyingi wapo
katika hatari za kupoteza usikivu.
“Changamoto ni kubwa sana hasa
kwa watu wenye umri kati ya miaka 18-45 ambapo wengi wao wameathiriwa
na sababu mbalimbali lakini sababu kubwa ni kelele zilizopitiliza”
Kambi
hiyo maalumu ya upimaji wa usikivu inafanyika ikiwa kuelekea kilele cha
maadhimisho ya siku ya usikivu duniani inayoadhimishwa tarehe 3 Machi
kila mwaka, mwaka huu imebeba kauli mbiu isemayo 'ili usikie vizuri
maishani mwako sikiliza kwa taadhali'.
No comments:
Post a Comment