Mkoa
wa Iringa wenye kumiliki asilimia 40 ya misitu ya kupandwa nchini
Tanzania na ni moja ya sehemu zenye aridhi bora sana kwa ajili ya kilimo
cha miti duniani. Ili kutumia fursa hii mkoa wa Iringa umeandaa
kongamano kubwa la uwekezaji katika sekta ya misitu.
Akifungua
kongamano hilo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa pongezi kubwa kwa
mkoa na pia kueleza msimamo wa Serikali ya awamu ya sita katika
kuchochea uwekezaji nchini. Pia Waziri Mkuu aliagiza makampuni yenye
kuchakata mazao ya misitu kuhakikisha yanatengeneza bidhaa bora na
kutosafirisha bidhaa ghafi.
Waziri
Mkuu aliuelezea mkoa wa Iringa kama eneo bora la uwekezaji likiwa na
muunganiko mzuri wa barabara na muda mfupi ujao kwa ndege baada ya
kukamilika kwa uwanja wa ndege wa Iringa.
Mkuu
wa Mkoa wa Iringa Queen Sendega alisema mkoa wake uko tayari kusaidia
wafanya biashara kufanya biashara kwa urahisi kwa kuweka mazingira
wezeshi.
Kabla
ya kufungua kongamano hilo alizindua chapa ya Iringa woodland ikiwa ni
lengo la mkoa wa Iringa kuchagiza ukuaji wa utengenezaji wa bidhaa za
mbao, kuutangaza mkoa na pia utalii.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi huo Mkurugenzi Mkuu wa Gofin Ventures Imani Kajula
ambao ni waandaaji wa kongamano hilo na mkakati wa kujenga chapa ya
Iringa woodland alisema " hii ni fursa pana kwa mkoa wa Iringa kufaidika
na sekta ya utalii, misitu na pia kuutangaza mkoa wa Iringa ndani na
nje ya Tanzania" pia kutoa ajira kwa vijana ambao watatumia chapa ya
Iringa woodland kutengeneza bidhaa mbali mbali
No comments:
Post a Comment