Ingawa matumizi ya pesa taslimu bado ni makubwa nchini, maendeleo ya malipo kufanyika kidijitali yanaridhisha huku Benki ya NMB ikichangia mafanikio hayo kwa kiasi kikubwa.
Mwishoni
mwa juma lililopita mchango wa NMB kwenye harakati za kuifanya Tanzania
iwe nchi ya uchumi wa kidijitali ulitambuliwa kimataifa na kampuni ya
Mastercard International.
Kampuni
hiyo kigogo wa teknolojia bunifu duniani iliitunuku NMB tuzo maalum
kutambua uwekezaji inayoufanya kusaidia kupunguza matumizi na kutegemea
sana pesa taslimu.
NMB ilipewa tuzo hiyo baada ya kuibuka benki kiongozi wa kukuza na kuhamasisha matumizi ya kadi za malipo za Mastercard nchini.
Tuzo
hiyo pia inadhibitisha kujitolea kwa NMB kuziimarisha huduma jumuishi
za kifedha na kuwa mstari wa mbele kuweka misingi madhubuti ya mifumo ya
malipo ya kidijitali.
Nishani
iliyopewa NMB na Mastercard Ijumaa jijini Dar es Salaam ni baada ya
kufanikiwa kukuza matumizi ya malipo ya kadi kwa kasi kubwa sana.
Katika
kufanya hilo, NMB ilivunja rekodi yake yenyewe ya kiasi cha pesa
kilichotumika katika vituo vya mauzo kwa kutumia kadi huku thamani ya
matumizi hayo ikiongezeka kwa asilimia 30 ndani ya mwaka mmoja.
Kwa
mujibu wa Mastercard, ni NMB pekee nchini na katika ukanda huu ambayo
imefanikiwa kuongeza matumizi ya kadi za malipo kwa zaidi ya asilimia
100 katika kipindi cha miezi 12.
Afisa
Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa benki hiyo, Bw. Filbert Mponzi,
alisema mafanikio yaliyoifanya NMB kuibuka kidedea yalipatikana kati ya
Juni 2020 na Juni 2021.
“Tuzo
hii ni kielelezo tosha kabisa cha ukubwa wa Benki ya NMB nchini
inayochagizwa na upana wa mtandao wake wa matawi 226 na wateja zaidi ya
milioni nne,” kiongozi huyo alinena kabla ya kupokea tuzo ya Mastercard.
“Hii
ni tuzo ya kwanza ya namna hii kuwahi kutolewa kwa benki hapa nchini
Tanzania. Asanteni sana wenzetu wa Mastercard na pia shukrani nyingi kwa
wateja wa NMB waliotufanya kutambuliwa na Mastercard,” Bw. Mponzi
alisema.
Sababu
zilizopelea ushindi huu wa kidijitali wa NMB ni mbili. Kwanza ni idadi
kubwa zaidi ya wateja wanaotumia kadi kuliko benki yoyote nchini. Zaidi
ya wateja wa NMB milioni tatu wanatumia kadi za Mastercard kwa ajili ya
huduma mbalimbali za kifedha idadi ambayo haijafikiwa na benki nyingine
zote nchini.
Bw.
Mponzi alisema sababu ya pili ni kiasi kikubwa cha pesa kilichotumika
katika vituo vya malipo kwa kutumia kadi za NMB MasterCard ambacho
kiliongezeka kwa asilimia 104 ndani ya mwaka mmoja.
“Mbali
na sababu hizi, Benki ya NMB imekuwa kinara katika kuhamasisha matumizi
ya kadi sio tu kwa ajili ya kutolea pesa katika ATM bali na katika
matumizi mengine mengi kama kufanya malipo katika sehemu za migahawa,
supermarket, vituo vya mafuta na katika sehemu za starehe na hata
kuagiza bidhaa mbalimbali kupitia mitandao.”
Bw
Mponzi alisema kutambuliwa mchango wa NMB kwenye mafanikio ya nchi
kidijitali ni sifa nyingine ya taasisi hiyo kutokuwa na mpinzani sokoni
na tuzo ya Mastercard ni moja ya nyingi za ubora ilizotunukiwa mwaka
huu.
Aidha,
alisema NMB pia ni mahili katika maeneo mengine kama kuongoza kupata
faida pamoja na kuwa na kiasi kikubwa cha amana na rasilimali fedha.
Ili
kuendeleza uongozi huo, Bw Mponzi aliweka wazi mikakati ya NMB kwa
ajili ya hilo akisisitiza kuepukana na ubaili kwenye uwekezaji na
umuhimu wa ubunifu.
“Benki
ya NMB itaendelea kubuni suluhisho mbalimbali zenye lengo la kuboresha
matumizi ya kadi na kwa kutumia teknolojia mbalimbali,” alibainisha
“Ni
imani yetu kuwa idadi ya watumiaji wa kadi itazidi kuongezeka na hata
miamala kupitia kadi itaongezeka zaidi,” aliongeza na kuisifia
Mastercard kwa ubobezi wake katika teknolojia ya kadi za malipo.
Mwaka
2014, NMB na Mastercard walikubaliana kushirikiana kutumia malipo ya
kielektroniki kuchochea uchumi wa kidijitali na kuwa sehemu ya ajenda ya
taifa ya kufanikisha huduma jumuishi za kifedha.
Meneja
wa MasterCard Afrika Mashariki, Bw Shehryar Ali, alisema tuzo ya NMB ni
zaidi ya kuwezesha matumizi ya kadi kwani benki hiyo imefanya mengi
kusaidia kupunguza matumizi ye pesa taslimu na kuendeleza huduma za
kifedha nchini.
“Matumizi
ya pesa taslimu ambayo yanafikia hadi asilimia 90 ya miamala yote
inayofanyika Tanzania yanaughalimu uchumi wa nchi asilimia mbili za pato
la taifa kwa sababu lazima pesa hizo zichapishwe, zihifadhiwe,
zisafirishwe na zilindwe,” Bw Ali alifafanua.
Afisa
Mkuu wa Biashara na Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi
(wapili kulia) akionyesha Tuzo ya MasterCard iliyokabidhiwa kwa Benki ya
NMB na Mkurugenzi Mkazi wa Afrika Mashariki wa MasterCard, Shehrya
Ali wakati wa hafla iliyofanyika Dar es Salaam.Kulia ni Mkuu wa
Biashara ya Kadi wa Benki ya NMB, Philbert Casmir na kushoto ni Mkuu wa
Biashara wa Master Card, Victor Ndlovu.
No comments:
Post a Comment