Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze
WALIMU
na wazazi wameaswa kushirikiana kuwasimamia wanafunzi wenye vipaji
maalum ikiwa ni pamoja na wanaomudu masomo ya sayansi, katika shule za
msingi ili kufikia elimu ya sekondari na kukuza taaluma zao.
Aidha jamii imetakiwa kuunga mkono juhudi za serikali kutatua changamoto mbalimbali kwenye sekta ya elimu pasipo kuiachia pekee.
Akizungumza
na walimu ,wageni, wanafunzi na viongozi mbalimbali kwenye mahafali ya
shule ya msingi Chalinze Modern Islamic, kwa niaba ya mgeni rasmi mbunge
wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete, mkuu wa sekondari
Lugoba,Abdallah Sakasa alibainisha, elimu ndio nguzo kwa watoto wetu.
Alisema
wanafunzi wanaofanya vyema shule za msingi wanapaswa kusimamiwa ili
kuepuka na masuala yasiyofaa ambayo yanaweza kuwaharibia mwanzo wao
mzuri waliouanza.
Hata
hivyo, Sakasa aliiasa jamii kushirikiana na serikali kuboresha na
kutatua changamoto za kielimu ikiwemo majengo ya madarasa.
"Ridhiwani
amewaomba wazazi kufanya jitihada ya Kujenga shule ya sekondari shule
hapa ,ili kusogeza upatikanaji wa elimu ya sekondari karibu na ameahidi
kuchangia mifuko ya saruji 50 na kokoto Lori mbili "alifafanua.
Hata
hivyo Sakasa alisema, ofisi ya mbunge kwa kushirikiana na mamlaka
nyingine watasimamia miradi ya maji inayoendelea ili shule ya Chalinze
Modern Islamic iondokane na changamoto ya ukosefu wa maji ya uhakika.
Mkuu
wa shule hiyo, Amran Bakari alieleza ,shule hiyo imeanzishwa mwaka 20,
kwasasa kuna jumla ya wanafunzi 575 ambapo 272 Ni wanafunzi wa kiume na
301 wasichana.
Awali
mkurugenzi wa Kimara Islamic center (KIC) inayosimamia Chalinze modern
Islamic na Matangini Islamic sekondari,Abdul Kiriwe alifafanua ,shule
hizo zinatoa elimu bora na kusimama maadili mema.
Aliwaomba
wazazi, kuwaendeleza watoto hao elimu ya sekondari na kusimama kwenye
maadili ya dini na kuwachunga ili wasipotee kitabia.
Kiriwe
alisema,wamebeba dhamana ya kumsomesha mwanafunzi aliyetoa mada ya
sayansi (Embryolohy),Ghania A'Aziz kuanzia kidato cha kwanza hadi Cha
sita katika shule ya sekondari ya Matangini Islamic Kimara.
Nae
kiongozi wa dini, alhaj Hamis Nassor aliwaomba wazazi na walezi kuunga
mkono ujenzi wa kuanzisha shule ya sekondari ilihali wanafunzi
wanaoanzishiwa mwanzo mzuri shuleni hapo waendelee na sekondari katika
shule hiyo.
Katika kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari Chalinze Modern Islamic ,imepatikana milioni zaidi ya 11.
No comments:
Post a Comment