Bondia Hassan Mwakinyo na Muargentina Jose Carlos Paz wametamba kila
mmoja atamchapa mwenzake katika pambano la kuwania ubingwa wa uzito wa
super-welter wa mabara unaotambuliwa na chama cha WBF.
Mwakinyo na Paz watapambana Ijumaa kwenye ukumbi wa Next Door Arena katika pambano lililopangwa kuwa la raundi 12.
Akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari jana, Mwakinyo alisema kuwa
atahakikisha Paz anaachana na mchezo wa ngumi za kulipwa kutokanana
kipigo alichumuandalia.
“Natamani
pambano lifanyike mapema iwezekanavyo, hata siku moja kabla kwani nipo
fiti zaidi ya nilivyokuwa mwanzoni. Sitaki kuwanyong’onyesha Watanzania
katika pambano hilo,” alisema Mwakinyo.
Alisema
kuwa anajua kuwa Paz ni bondia mzuri na amejiandaa vyema katika pambano
hilo, lakini kutokana na jinsi alivyojiandaa, hatakuwa na nafasi ya
kutamba kwake.
Kwa upande wake, Paz alisema kuwa hakuja nchini kutembea zaidi ya kuwania ubingwa wa ambao Mwakinyo anao.
“Nipo
vizuri, mazoezi yangu nchini yamekuwa na mafanikio makubwa na hali ya
hewa siyo tatizo. Nitamfundisha ngumi Mwakinyo ,” alisema Paz.
Kwa
mabondia hao kutambiana pia bondia Hussein Itaba na mpinzani wake
kutoka DR Congo, Alex Kabangu, Fatuma Zarika dhidi ya Patience Mastara
(Zimbabwe) na Mtanzania Zulfa Macho ambaye atazichapa na Alice Mbewe wa Zambia pia walitambiana.
Mkurugenzi
wa Jackson Group Sports, Kelvin Twissa alisema kuwa maandalizi
yamekamilika na kuwaomba mashabiki kuendelea kununua tiketi kwa ajili ya
pambano hilo.
“Maandalizi
yapo vizuri na kama mnavyoona mabondia wote wapo hapa na sas
tunamsubiri Rais wa WBF, Howard Goldberg na mwamuzi Edward John Marshall
ambao watawasili leo Jumatano Novemba 11,” alisema Twisa.
Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya Jackson Group Sports Kelvin Twissa
akiwatambulisha Hassan Mwakinyo na Jose Carlos Paz ambao watawania
mkanda wa mabara wa chama cha WBF wa uzito wa super-welter.
Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya Jackson Group Sports Kelvin Twissa
akiwatambulisha Hussein Itaba wa Tanzania (kulia) na Alex Kabangu wa DR
Congo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya Jackson Group Sports Kelvin Twissa
akiwatambulisha Alice Mbewe wa Zambia (kulia) na Zulfa Macho wa
Tanzania.
Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya Jackson Group Sports Kelvin Twissa
akiwatambulisha Fatuma Zarika wa Kenya na Patience Mastara wa Zimbabwe .
No comments:
Post a Comment