HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 28, 2020

CCM YAZINDUA AWAMU YA TATU YA KAMPENI ZAO, AWAMU YA NNE KUZINDULIWA ZANZIBAR

 

Mgombea Mwenza wa CCM na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye uzinduzi wa awamu ya tatu ya Kampeni za chama hicho wilayani Kongwa leo.
Mbunge Mteule wa Kongwa na Spika wa Bunge,Job Ndugai akihutubia kwenye kampeni za CCM katika eneo la Mkoka wilayani Kongwa.
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally akizungumza katika mkutano wa kampeni katika eneo la Mkoka wilayani Kongwa, Dodoma.
Mbunge wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Dodoma, Alhaji Adam Kimbisa akiwapungia mkono wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni katika eneo la Mkoka wilayani Kongwa ambapo chama hicho kimezindua awamu ya tatu ya kampeni zake.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mgombea Ubunge wa Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dodoma, Mariam Ditopile walipokutana kwenye uzinduzi wa awamu ya tatu ya kampeni za CCM leo.

Charles James, Michuzi TV
CHAMA cha Mapinduzi CCM leo kimezindua kampeni zake kwa awamu ya tatu huku ikisema wana uhakika wa kuibuka na ushindi kwenye kura za Urais, Wabunge na Madiwani kwa asilimia 89.

Uzinduzi huo umefanyika katika eneo la Mkoka wilayani Kongwa ambapo mgeni rasmi Mgombea Mwenza na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Bashiru Ally, Spika wa Bunge na mbunge mteule wa Kongwa, Job Ndugai.

Akizungumza katika mkutano huo, Mama Samia amewaomba watanzania kujitokeza kwa wingi Oktoba 28 kwenda kupiga kura kwa wagombea wa CCM ili kutengeneza mafiga matatu yatakayowatumikia kwa miaka mitano mingine.

Amesema imani waliyopewa kwa miaka mitano na wananchi imewafanya wafanye kazi kubwa ya kuwatumikia na kuomba waiamini tena CCM kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

" Tumefanya mambo makubwa sana hapa Kongwa na Tanzania kwa ujumla, hakuna eneo ambalo halijaguswa tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto na kufanya maboresho kwenye nyanja mbalimbali.

Leo hii Kongwa kila kijiji kina umeme, na awamu ijayo tumepanga kuhakikisha kila nyumba inakua na umeme, sekta ya afya, miundombinu, elimu na nishati. Mkituamini na kutuchagua tena tutafanya zaidi ya awamu ya kwanza," Amesema Mama Samia.

Kwa upande wake Katibu Mkuu, Dk Bashiru Ally amesema uzinduzi huu wa awamu ya tatu una mikakati Maalum kuliko awamu mbili ile ya kwanza Dodoma na ya pili iliyozinduliwa mkoani Kagera.

Amesema awamu ya nne wataizindua visiwani Zanzibar na wanazo awamu sita tofauti ambazo zimebeba mikakati na mbinu mahususi za kushinda uchaguzi huo.

" Nasikia wenzetu wanataka kuvua jezi wavalishane jezi moja, wanaangaika kama wendawazimu, wamepagawa na kuchanganyikiwa, sisi kazi ni moja tu kuwashinda bila kujali udhaifu wao.

Kila siku tuna mikutano 20 ya kampeni kitaifa kwa maana ya Mgombea Urais, Mgombea Mwenza na Mjumbe wa Kamati Kuu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, tuna mikutano 600 kila siku ya Wabunge na Madiwani, wenzetu hata hawaeleweki walipo, ni dhaifu kuliko nyakati zote," Amesema Dk Bashiru.

Nae Mbunge wa Kongwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai amemuahidi Mama Samia kuwa Kongwa itaongoza kwa kura kwa asilimia 100 na wala hakuna kura itakayoenda upinzani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad