Wataalam
wa Wizara ya Maji wakikagua maendeleo ya kazi ya ya uboreshaji wa
Chanzo cha Maji cha Mbwiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi,
mkoani Mtwara.
Mhandisi
Joshua Lawrence wa Wizara ya Maji akikagua baadhi ya mashine
zinazotumika katika Chanzo cha Maji cha Mitema katika Halmashauri ya
Wilaya ya Newala, mkoani Mtwara.
Kiongozi
wa Timu ya Wataalam wa Wizara ya Maji, Mkurugenzi Philipo Chandy
(aliyekaa) akiwa pamoja na Timu ya Wataalam ya Wizara ya Maji katika
Chanzo cha Maji cha Mbwinji katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi,
mkoani Mtwara.
Afisa
Maendeleo ya Jamii wa Wizara ya Maji, Prisca Henjewele akitoa elimu kwa
msimamizi wa miongoni mwa vituo vya kuchotea maji vya Mradi wa Maji wa
Lukuledi unaotoa huduma kwa wakazi 17,060 katika vijiji 5 vya
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, mkoani Mtwara.
Miongoni mwa vituo vya Mradi wa Maji wa Lukuledi vikitoa huduma katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, mkoani Mtwara.
Ujenzi wa tenki la Mradi wa Maji wa Mnolela ukiendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala, mkoani Mtwara.
…………………………………………………………………………..
Serikali
imetenga kiasi cha Sh. Bilioni 24 kwa ajili ya kazi ya ujenzi wa miradi
ya maji katika vijiji 205 ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa ahadi ya
kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa maeneo ya
vijijini mkoani Mtwara, ambao kati yao asilimia 60.1 wanapata huduma.
Meneja
wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA)
mkoa wa Mtwara, Mhandisi Mbaraka Ally amesema fedha hizo zimetengwa kwa
ajili ya utekelezaji wa miradi 31 itakayonufaisha wakazi zaidi ya
300,000 katika vijiji 205 kwa mwaka huu wa fedha wakati akitoa taarifa
kwa Wataalam wa Wizara ya Maji wakiwa katika ufuatiliaji na kutathmini
ujenzi wa miradi ya maji ya Kilidu Mnui na Mnolela katika Wilaya ya
Newala.
“Kati
ya Sh. bilioni 24 zilizotengwa, tumeshapokea Sh. bilioni 8 na zimeanza
kutumika kwenye ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kilidu Mnui ambao
umeshakamilika kwa gharama ya zaidi ya Sh. bilioni 1.4, ukiongeza lita
720,000 kwa siku na kuhudumia wanachi 60,000 wa Newala mjini na vijiji
jirani, changamoto iliyopo ni umeme ambapo tayari tumeshachukua hatua ya
kubadilisha mita ya LUKU na baada ya muda mfupi mradi utaanza kutoa
huduma’’, alisema Mhandisi Ally.
“Vilevile
Mradi wa Maji wa Mnonela umefikia asilimia 45 na utakamilika mwezi
Disemba, 2020 kwa gharama ya zaidi ya Sh. milioni 400 na kuhudumia
wakazi 2,805 wa vijiji vya Dodoma, Mkunjo, Mtanda na Mnonela katika
Halmshauri ya Wilaya ya Newala inayopata huduma ya maji kwa asilimia
55”, alifafanua Mhandisi Ally.
Aidha,
wakazi 17,060 wa vijiji vya Lukuledi, Nasindi, Polapola, Kalinga na
Napata wameanza kupata huduma ya majisafi na salama mara baada ya Mradi
wa Maji wa Lukuledi kukamilika kwa asilimia 95 kwa kiasi cha zaidi ya
Sh. milioni 600 na kumaliza kilio cha muda mrefu.
Mkurugenzi
wa Huduma ya Ubora wa Maji, Philipo Chandy ameipongeza Mamlaka ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Masasi-Nachingwea (MANAWASA) kwa kazi ya
uboreshaji wa Chanzo cha Maji cha Mbwiji katika Halmashauri ya Wilaya ya
Masasi.
Amesema
kuwa maendeleo ya ujenzi ni mazuri na utakapokamilika utaimarisha zaidi
huduma ya maji kwa wananchi waishio katika wilaya za Masasi mkoani
Mtwara, Nachingwea na Ruangwa mkoani Lindi.
No comments:
Post a Comment