HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 30, 2019

Dk Mahiga ataka weledi upashanaji habari

 Mgeni rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Dk Augustine Mahiga (katikati) akiwa ameongozana na Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo (kushoto), Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Nancy Kaizilege (kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya TADIO, Maimuna Msangi pamoja na Mwenyekiti wa MISA Tanzania, Salome Kitomari mara baada ya kuwasili kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Mshehereshaji ambaye pia ni mkufunzi wa Redio za Jamii, Rose Haji Mwalimu akitambulisha meza kuu (haipo pichani) wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Kutoka kushoto meza kuu ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Nancy Kaizilege, Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo, Mgeni rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Dk Augustine Mahiga, Mwenyekiti wa MISA Tanzania, Salome Kitomari pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya TADIO, Maimuna Msangi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Mgeni rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Dk Augustine Mahiga akizungumza na wadau wa tasnia ya habari na waandishi kutoka vyombo vya mbalimbali vya habari jamii nchini wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo akitoa salamu za Mkuu wa mkoa wa Morogoro wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Nancy Kaizilege akitoa salamu za UNESCO kwa niaba ya Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika hilo nchini, Tirso Dos Santos (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Mwenyekiti wa Bodi ya TADIO, Maimuna Msangi akitoa salamu za TADIO wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Mwenyekiti wa MISA Tanzania, Salome Kitomari akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Ofisa habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa hapa nchini (UNIC), Didi Nafisa akiendesha majadiliano wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Baadhi ya wadau wakongwe katika tasnia ya habari nchini wakiwasilisha maoni wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Baadhi ya waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya Redio Jamii na wadau wa tasnia ya habari nchini walioshiriki maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
Mgeni rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Dk Augustine Mahiga na meza kuu katika picha ya pamoja na Sekretarieti iliyofanikisha maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
Mgeni rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Dk Augustine Mahiga na meza kuu katika picha ya pamoja na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya Redio Jamii na wadau wa tasnia ya habari nchini walioshiriki maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.
 Maafisa kutoka Umoja wa Mataifa Rose Mwalongo (wa pili kushoto) na Stella Vuzo (wa pili kulia) katika picha ya kumbukumbu na wadau wa tasnia ya habari nchini wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Morogoro Hoteli mkoani Morogoro.

Na Mwandishi Wetu, Morogoro
SERIKALI kwa kutambua umuhimu wa upatikanaji wa taarifa imesema ipo tayari kuangalia vikwazo vinavyosababisha ukosefu wa taarifa sahihi, ikiwamo sheria ili uchakataji wa habari uboreke kwa manufaa ya taifa.
Aidha imesema kwamba inatambua matatizo mengi duniani yanayosababisha uhasama yanatokana na kukosekana taarifa sahihi miongoni mwa wanadamu.
Aidha kukosekana kwa taarifa sahihi na kuwapo kwa taarifa za uongo kumesababisha kuwapo kwa vita na usumbufu mwingine ambao ungeliweza kutatuliwa kwa kuwapo kwa taarifa zilizo sahihi.
Kauli hizo zimetolewa na Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Augustine Mahiga kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upataji Taarifa iliyoadhimishwa mkoani Morogoro hapa nchini yakiwa na kauli mbiu “Upataji Taarifa : Asiachwe Mtu!”.
Alisema ili taifa la Tanzania lisiingie katika migogoro serikali ipo tayari kusikiliza wadau na kushirikiana nao kuweka mazingira ya upatikanaji wa taarifa kuwa bora zaidi na unaojali maslahi mapana ya nchi.
Pamoja na kuwapongeza waandazi wa hafla hiyo, UNESCO,  Dk. Mahiga pia alielezea umuhimu wa taasisi za umma na binafsi zinazohusika na upashaji habari kuifanya kazi hiyo kwa uaminifu na weledi mkubwa ili kuondoa matatizo yanayoambatana na kukosekana kwa habari.
Alisema uchakataji wa habari ni muhimu ili wananchi wote waweze kupata habari na kuzitumia kwa maendeleo yao.
Alisema suala la upatikanaji wa taarifa sahihi si wa taifa moja tu bali dunia nzima na hilo limehimizwa tangu kumalizika kwa vita ya pili ya dunia ambayo kwa namna fulani ilichochewa na kukosekana kwa habari sahihi.
Alisema pamoja na dunia mataifa kuridhia haki ya kujieleza na kupata habari, mataifa na watu wengi wamekuwa wakikosa au wakinyimwa haki ya kuhabarishwa na hivyo kuzua matatizo katika jamii husika.
Alisema ndio maana Tanzania imekuwa moja ya nchi iliyotia saini mikataba uhuru na haki ya kupata habari na kutamka wazi katika katiba yake kuhusu haki za habari.
Alisema kuna manufaa makubwa kwa watu kuwa huru katika kuhabarishana kama kuongeza uelewa wa jamii katika masuala mbalimbali yakiwemo ya afya uchumi na namna ya kuishi.
Hata hivyo alisema taarifa zinapokuwa mbaya na zisizojenga husababisha migogoro na migongano katika jamii na hivyo kuitaka jamii kuhakikisha kwamba inapata taarifa sahihi na zenye kujenga jamii husika.
Alisema kwa kuwa utawala bora unahusisha na demokrasia ni vyema kwa nchi yoyote inayojinadi kuwa na demokrasia ni lazima kuwa na jukwaa kwa wananchi wake kupata habari sahihi.
Waziri huyo alisema kwamba habari ni kama upanga wenye makali pande zote unaoweza kuleta neema au balaa .
“Habari zikitumika vyema zinaleta haki na zikitumika vibaya zinaleta migogoro na kuhatarisha usalama wa nchi“ alisema Dk. Mahiga.
Alipotolea mfano wa uchaguzi wa serikali za mitaa na kusema kwamba ili wananchi waweze kuufanya kwa ufanisi mkubwa ni lazima wawe wameelimishwa vya kutosha kutambua na kujitambua ili wapige kura zenye uhakika.
Alipongeza Mtandao wa Radio za Jamii (TADIO) kwa kuwa karibu na wananchi na kusema wanafanyakazi njema ya kuhabarisha jamii hasa kutokana na ukweli kuwa radio ya taifa haifiki kila mahali.
Alisema kazi inayofanywa na TADIO ni ya muhimu kwani inasaidia serikali katika kuelimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo na hasa mwelekeo kama taifa.
Alisema kutokana na ufanisi huo ni vyema taasisi hizo zikajikita katika kueleza ukweli kwa weledi mkubwa ili wasiingie katika mtego wa kusumbuana na sheria na hivyo kurejesha nyuma matunda muhimu ya haki za kupashana habari.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TADIO, Maimuna Msangi akizungumza kabla ya Waziri Mahiga alishukuru Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kuwezesha kuwepo kwa tukio hilo muhimu hapa nchini.
Aidha alishukuru kuwapo kwa makubaliano ya awali kati ya TADIO na Chuo Kikuu Huria yaliyowezesha Mtandao huo wa Redio Jamii kuwa na ofisi katika majengo ya chuo hicho.
Pia alishukuru UDOM kwa kuruhusu mifumo yake ya Tehama kutumika na kuja kuwa sehemu ya mafunzo kwa wanahabari.
Pia alishauri taasisi zote husika kuona changamoto zinazokabiliwa na redio jamii na kuzishughulikia.
Naye Mwenyekiti wa MISA Tanzania, Salome Kitomari akizungumza alisema kwamba nchi zilizoendelea zimefanikiwa kutokana na kutumia vyema haki ya upashanaji habari.
Alisema hata hivyo hali bado si nzuri kwa upande wa watumishi wa umma ambao wamekuwa wagumu kutoa taarifa mbalimbali zinazohitajika na vyombo vya habari kwa ajili ya kufikisha kwa umma.
“ Kumekuwa na usiri mkubwa katika miradi mbalimbali ya maendeleo na kuleta sintofahamu” alisema Kitomari.
Alitoa wito kwa watumishi wa umma kujengewa uwezo ili waweze kushiriki kikamilifu katika suala zima la uchakataji habari.
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Nancy Kaizilege alisema katika hotuba aliyosoma kwa niaba ya Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Tirso Dos Santos kwamba shirika hilo linaridhishwa na kasi ya TADIO na kutaka wananchi kutambua haki zao za msingi za kupashana habari na kufanya hivyo kwa weledi.
Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa alisisitiza umuhimu wa kutumia habari kuharakisha kasi ya maendeleo.
TADIO – Tanzania Development Information Organisation ni asasi ya habari za maendeleo Tanzania inayohusisha vyombo vya habari za kieletroniki yaani Radio zinazozalisha maudhui ya kijamii ambazo nyingi hupatikana mikoani na sehemu za vijijini ambako idadi kubwa ya Watanzania wanaishi.
TADIO ina jumla ya Radio wanachama 32 katika mikoa yote ya Tanzania bara na visiwani isipokuwa Tabora na Singida. Uwezo wa Radio Jamii hizi kufikia watanzania waliopo mikoani na hasa vijijini hukadiriwa kufikia asilimia 70%.
TADIO ilianzishwa rasmi mwaka 2017 baada ya kuvunjika kwa asasi ya mfanano ya awali iliyojulikana kama COMNETA.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad