HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 10, 2019

MEYA MWITA AMWAGA VIFAA VYA KUJIFUNGULIA WAKINA MAMA HOSPITALI ZA JIJI LA DAR

MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita , leo (jana) amekabidhi vifaa vya kujifungulia wakina mama (Delivery Pack) katika Hospital za jijini hapa ikiwa ni sehemu ya kuwasaidia wa kimama wenye hali hiyo.

Hospital zilizopatiwa vifaa hivyo ni Mnazi mmoja iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Ilala,ambapo imepewa vifaa hivyo 300 na zile zilizopo katika Halmashauri ya Kigamboni.

Akizungumza na wauguzi katika hospitali hiyo,Mstahiki Meya Mwita aliagiza kuwa vifaa hivyo vitolewa bure kwa wakina mama wenye uhitaji na kuagiza hospital hizo zisiwauzie.
 Alifafanua kuwa wakina mama wajawazito wanapaswa kuthaminiwa na kwamba sio wote wenye uwezo wa kununua vifaa hivyo na kushauri wenye uwezo kuwasaidia.

Alifafanua kuwa serikali kwa kiasi kikubwa imekuwa ikijali wakina mama wajawazito na kushauri kuwa kama wadau wa maendeleo wanapaswa kushirikiana na serikali kuwalinda wa mama wajawazito.
 “ Ukiangalia serikali inatilia mkazo jambo hili, inajali wakina mama na kuhakikisha kuwa wanajifungua salama, wote tunapaswa kujali maisha yao, nijukumu letu kulinda mama mjamzito “ alisisitiza.

Changamoto ni nyingi,uhitaji wa vifaa ni mkubwa kutokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya wakina mama wanaojifungua,nitoe rai kuwa hili ni jukumu la kila mmoja wetu kuisaidia serikali” aliongeza.

Alisema “Wakina mama ni watu wamuhimu sana katika Taifa hili, tunapaswa kuwaheshimu na kuwathamini, pia wanakazi kubwa ambayo kwao inachangamoto, lakini kama viongozi na wadau wengine tunajukumu la kuwasaidia” alisema Meya Mwita.
“ Vifaa hivi najua havitoshi kulingana na Idadikubwa mliyonayo katika Hospitali hii, ila niwaombe muwapatie bure msiwauzie, huu ni msaada kwao, napindi tutakapopata nyingine tutawaletea” aliongeza.

Katika hatua nyingine, Meya Mwita ameipongeza hospitali hiyo kutokana na huduma wanazozitoa na hivyo kuwasihi kuendelea na utoaji mzuri wa huduma hiyo.

Mganga Mfadhiwi wa Hospitali hiyo Sophinias Ngonyani alimpongeza Meya Mwita kwakutoa vifaa hivyo na kusema kuwa zitawasaidia wakina mama na kusisitiza kwamba watazigawa bure kama walivyoagizwa.

Alisema kuwa hospitali hiyo imekuwa ikihudumia wakina mama wajazito kutoka sehemu mbalimbali jijini hapa kwani hali hiyo imetokana na huduma nzuri wanazozitoa.

Aliongeza kuwa hospital hiyo inazingatia utoaji huduma bora kama ambavyo serikali inasisitiza kila wakatii jambo ambalo alisema limepelekea kuwa na idadi kubwa ya wakina mama wanaojingulia katika hospitali hiyo.

“ Tunampongeza Mstahiki Meya kwa kutupatia vifaa hivi, tunauhitaji mkubwa kulingana na idadi ya wakinamama wanaojifungua hapa kwetu, ametusaidia sana tunampongeza” alisema.

Hata hivyo vifaa hivyo vitaendelea kutolewa kwa hospitali nyingine zilizopo jijini hapa ,huku nyingine zikichukuliwa katika ofisi ya Mstahiki Meya.

Vifaa hivyo vimetolewa na Mstahiki Meya wa jiji kwa kushirikiana na Kampuni ya usafirishaji abiria kwa njia ya mtandao ya Bolt vyenye thamani ya shilingi milioni 25.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad