HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 24, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI NA RAIS MSTAAFU KIKWETE WAONDOKA NCHINI KUUDHURIA SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA RAIS MPA WA AFRIKA YA KUSINI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo wakati akiondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kuelekea Afrika ya Kusini asubuhi hii ambapo kesho atahudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa nchi hiyo Mhe. Cyril Ramaphosa mjini Pretoria.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete wakati wakiondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tayari kuelekea Afrika ya Kusini asubuhi hii ambapo kesho watahudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa nchi hiyo Mhe. Cyril Ramaphosa mjini Pretoria.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameongoza na na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu wa Rais wa CCM (Bara) Ndg. Philip Mangula wakipanda kwenye ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam tayari kuelekea Afrika ya Kusini asubuhi hii ambapo kesho watahudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa nchi hiyo Mhe. Cyril Ramaphosa mjini Pretoria. Picha na IKULU

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad