HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 21, 2019

RAIA WA KENYA APANDISHWA KIZIMBANI KWA KESI YA UHUJUMU UCHUMI

  Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii
RAIA wa Kenya, ambae ni mtaalamu IT, Brian Lusiola na Meneja Uwendeshaji wa Biashara wa Kampuni ya Inventure Mob Tanzania Ltd, Ahmed Ngassa wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi, likiwemo la kuingiza  kifaa cha mawasiliano nchini bila kibali cha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kuisababishia Serikali hasara ya Sh milioni 64.2.

Mbali na Lusiola na Ngassa mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Kampuni ya Inventure Mobile Tanzania Ltd inayowafanya biashara na Tala Tanzania.

Akisoma hati ya mashtaka leo Machi 21,2019,  Wakili wa Serikali Mwandamizi, Jackline Nyantori amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi kuwa, washtakiwa wametenda makosa hayo, wakiwa katika jengo la Tanzanite Park, lililopo katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam huku wakijua ni kinyume cha sheria.
Imedaiwa, katika shtaka la kwanza kuwa, katika tarehe isiyofahamika kati ya Januari Mosi na Desemba 31, 2018 washtakiwa wakiwa katika jengo hilo kinyume na sheria waliingiza kifaa cha mawasiliano kinachoitwa Proliant MLI GEN 9 Server (PABX Virtual Mashine yenye serial number 76520D88838129_425) bila kuwa na leseni kutoka TCRA.

Katika shtaka la pili,  imedaiwa siku na mahali hapo,  washtakiwa pamoja na kampuni hiyo, walisimika kNa Karama Kenyunko, Globu ya Jamii.
RAIA wa Kenya, ambae ni mtaalamu IT, Brian Lusiola na Meneja Uwendeshaji wa Biashara wa Kampuni ya Inventure Mob Tanzania Ltd, Ahmed Ngassa wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi, likiwemo la kuingiza  kifaa cha mawasiliano nchini bila kibali cha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kuisababishia Serikali hasara ya Sh milioni 64.2.

Mbali na Lusiola na Ngassa mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Kampuni ya Inventure Mobile Tanzania Ltd inayowafanya biashara na Tala Tanzania.

Akisoma hati ya mashtaka leo Machi 21,2019,  Wakili wa Serikali Mwandamizi, Jackline Nyantori amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi kuwa, washtakiwa wametenda makosa hayo, wakiwa katika jengo la Tanzanite Park, lililopo katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam huku wakijua ni kinyume cha sheria.

Imedaiwa, katika shtaka la kwanza kuwa, katika tarehe isiyofahamika kati ya Januari Mosi na Desemba 31, 2018 washtakiwa wakiwa katika jengo hilo kinyume na sheria waliingiza kifaa cha mawasiliano kinachoitwa Proliant MLI GEN 9 Server (PABX Virtual Mashine yenye serial number 76520D88838129_425) bila kuwa na leseni kutoka TCRA.

Katika shtaka la pili,  imedaiwa siku na mahali hapo,  washtakiwa pamoja na kampuni hiyo, walisimika kifaa hicho na kuendesha mtambo huo wa mawasiliano bila kuwa na leseni inayotolewa na TCRA.

Aidha  washtakiwa wanadaiwa, kutoka Januari 2 hadi  Machi 11,2019 waliendesha kifaa hicho cha kieletroniki cha mawasiliano kwa kurusu simu za kimataifa zilizoingia nchini bila kibali cha TCRA.

Katika shtaka la nne, washtakiwa hao wanadaiwa kumiliki kifaa hicho kilaghai, ambapo wakiwa na nia ya kukwepa gharama za uendeshaji wa kifaa kwa ajili ya kupokea na kusambaza mawasiliano, walisambaza simu hizo za kimataifa nchini.

Pia washtakiwa wanadaiwa kutumia kifaa hicho kilichounganishwa na mawasiliano kwa nia ya kupokea na kusambaza mawasiliano bila kupata kibali cha TCRA

Katika shtaka la sita, wakili Nyantori amedai kwa  matendo yao hayo ya makusudi, washtakiwa wameisababishia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na TCRA hasara ya Sh 64,260.000/-

Hata hivyo washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mhakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi ispokuwa kwa kibali kutoka kwa DPP.
kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na imeahirishwa hadi  Aprili 3,2019 kwa kutajwa.ifaa hicho na kuendesha mtambo huo wa mawasiliano bila kuwa na leseni inayotolewa na TCRA.

Aidha  washtakiwa wanadaiwa, kutoka Januari 2 hadi  Machi 11,2019 waliendesha kifaa hicho cha kieletroniki cha mawasiliano kwa kurusu simu za kimataifa zilizoingia nchini bila kibali cha TCRA.

Katika shtaka la nne, washtakiwa hao wanadaiwa kumiliki kifaa hicho kilaghai, ambapo wakiwa na nia ya kukwepa gharama za uendeshaji wa kifaa kwa ajili ya kupokea na kusambaza mawasiliano, walisambaza simu hizo za kimataifa nchini.

Pia washtakiwa wanadaiwa kutumia kifaa hicho kilichounganishwa na mawasiliano kwa nia ya kupokea na kusambaza mawasiliano bila kupata kibali cha TCRA

Katika shtaka la sita, wakili Nyantori amedai kwa  matendo yao hayo ya makusudi, washtakiwa wameisababishia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na TCRA hasara ya Sh 64,260.000/-

Hata hivyo washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mhakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi ispokuwa kwa kibali kutoka kwa DPP. Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na imeahirishwa hadi  Aprili 3,2019 kwa kutajwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad