Benki ya KCB Tanzania imefanya kongamano la kwanza ya Biashara
Club kwa mwaka 2019 jijini Arusha baada ya kuandaa kongamano kama hilo
jijini Mwanza mwishoni kwa mwaka 2018.
Zaidi ya kutoa elimu ya
usimamizi wa fedha, uendeshaji wa biashara na sheria za kodi, KCB
Biashara Club pia inawawezesha wafanyabiashara kupanua wigo wa biashara
zao kwa kuwakutanisha na wafanyabiashara wa nje na ndani ya nchi.
Tangu
kuzinduliwa kwake, KCB Biashara Club imeendelea kuonyesha dhamira yake
ya kukuza biashara kwa kutoa huduma bora za kibenki kwa wafanyabiashara
wadogo na wakati yaani (SME) pamoja na kuwaonyesha mbinu za kukuza
mitaji ya shughuli zao za kibiashara.
Kongamano hilo lilikuwa na
lengo mahususi la kukutanisha wadau mbali mbali katika sekta ya utalii
wakiwemo wafanyabiashara na lilifanyika katika sehemu mbili ambapo
sehemu yakwanza ilikuwa mahususi kwa wateja wa Benki ya KCB wapatao 250,
huku sehemu ya pili ikiwa ni jukwaa la wazi kwa wakazi wengine wa
Arusha kupata elimu ya huduma za kibenki kutoka kwa wataalam wa Benki ya
KCB.
Akiongea wakati wa kufungua kongamano hilo, Mkuu wa Masoko
na Mahusiano, Christine Manyenye alisema Benki ya KCB imefanya juhudi za
mahususi za kuwaleta wadau kama Tanzania National Parks Agency
(TANAPA), Tanzania Revenue Authority (TRA), Tanzania Association of Tour
Operators (TATO) and East Africa Business Council (EABC) kwa nia ya
kujadiliana jinsi ya kutatua baadhi ya changamoto na kupata njia muafaka
za kuendeleza sekta ya utalii nchini.
Kwa upande wake Meneja wa
Tawi, Benki ya KCB Arusha, Judith Lubuva aliwapongeza wafanya biashara,
wadau na wakazi wa Arusha kwa kuhudhuria kongamano. Aliongeza kwamba
kongamano hilo limefanyika kwa wakati muafaka ambapo sekta ya utalii
inaendelea kuimarika katika kanda ya kaskazini na Tanzania kwa ujumla.
Mkuu
wa Kitengo cha Wafanyabishara Wadogo na wa Kati (SME) Abdul Juma
aligusia fursa tofauti zinazoletwa na Biashara Club zikiwemo
kuwakutanisha wafanya biashara mbali mbali wa nje na ndani ya nchi,
kupanua wigo wa masoko kupitia safari za pamoja kwenda nchi kama China,
Malaysia na Afrika Kusini.
Juma aliwahakikishia wadau kwamba KCB
Bank ina dhamira ya kuinua sekta ya utalii kwa kuitambulisha Tour
Operator Account inayowezesha malipo ya kieletroniki pamoja na kuwana
faida zingine zikiwemo huduma kwa njia ya mtandao kuwa bure na kutoa
pesa bure.
Akiongea katika warsha hiyo, mwakilishi kutoka Mamlaka
ya Mapato (TRA), Ombeni Urio aliyekuwa mshauri wa masuala ya kodi,
alisisitiza umuhimu wa wafanya biashara hao kufuata kanuni za kodi.
Aliipongeza Benki ya KCB kwa kumualika ili aweze kutoa elimu hiyo ambayo
ilikuwa inahitajika kwa sana.
Mkuu wa Idara ya Masoko na Mahusaino Christine Manyenye akijibu maswali kutoka kwa wafanya biashara wa jijini Arusha katika kongamano lililohudhuriwa na wafanyabiashara zaidi ya 250 ikiwajumuisha wadau mbali mbali kutoka sekta ya utalii wakiwemo Tanzania National Parks Agency (TANAPA), Tanzania Revenue Authority (TRA), Tanzania Association of Tour Operators (TATO) and East Africa Business Council (EABC) kwa nia ya kujadiliana jinsi ya kutatua baadhi ya changamoto na kupata njia muafaka za kuendeleza sekta ya utalii nchini.
Afisa Masoko wa TANAPA Ernest Jackinda akiongea na wageni waalikwa katika warsha ya Biashara Club iliyohudhuriwa na wafanyabiashara zaidi ya 250 iliwajumuiasha wadau mbali mbali katoka sekta ya utalii wakiwemo Tanzania National Parks Agency (TANAPA), Tanzania Revenue Authority (TRA), Tanzania Association of Tour Operators (TATO) and East Africa Business Council (EABC) kwa nia ya kujadiliana jinsi ya kutatua baadhi ya changamoto na kupata njia muafaka za kuendeleza sekta ya utalii nchini.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Masuala ya Kibenki Masika Mukule akiongea na wageni waalikwa wakati wa maongezi ya ana kwa ana katika warsha ya Biashara Club iliyohudhuriwa na wafanyabiashara zaidi ya 250 iliwajumuiasha wadau mbali mbali katoka sekta ya utalii wakiwemo Tanzania National Parks Agency (TANAPA), Tanzania Revenue Authority (TRA), Tanzania Association of Tour Operators (TATO) and East Africa Business Council (EABC) kwa nia ya kujadiliana jinsi ya kutatua baadhi ya changamoto na kupata njia muafaka za kuendeleza sekta ya utalii nchini.
No comments:
Post a Comment