Wamiliki wa vyombo vya usafiri jijini Dodoma, wameshauriwa kuchangamkia fursa ya kutoa huduma ya usafiri kutoka maeneo mbalimbali ya jiji hilo kuelekea mji wa serikali ambako ofisi za serikali zinajengwa kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi na wadau wa serikali.
Ushauri huo umetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb), alipofanya ziara kuangalia maendeleo ya ujenzi wa ofisi yake katika mji wa serikali, Ihumwa ambayo iko kwenye hatua za mwisho kukamilika kwa ajili ya kutoa huduma.
Mhe. Mkuchika amesema, ofisi yake itaanza kutoa huduma siku chache zijazo, hivyo uwepo wa huduma ya usafiri ni muhimu sana, kwani itawawezesha wananchi kufika kwa urahisi kupata huduma ikiwa ni pamoja na kuwarahisishia watumishi wa ofisi yake na taasisi nyingine kufika kwa wakati katika maeneo yao ya kazi.
Aidha, Mhe. Mkuchika amezitaka taasisi zote za umma zinazojenga ofisi katika mji wa serikali, kuishirikisha Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) ili kupata ushauri wa kitaalamu wa namna bora ya kujenga miundo mbinu rafiki ya TEHAMA itakoyorahisisha utoaji huduma kwa umma. “Ni vema, taasisi zinazojenga ofisi katika mji wa serikali kuomba ushauri wa kitaalamu wa usimikaji wa miundombinu ya TEHAMA kabla ya kukamilisha ujenzi ili kuziwezesha taasisi hizo kuwa na mifumo ya TEHAMA ya utoaji huduma ya uhakika,” Mhe. Mkuchika amesisitiza.
Mhe. Mkuchika ameipongeza Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa hatua nzuri ya ujenzi iliyofikiwa na Menejimenti ya ofisi yake kwa usimamizi mzuri. Naye, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) ameridhishwa na ujenzi wa ofisi hiyo kwani umezingatia mahitaji muhimu ya kundi maalum kwa kuweka miundombinu rafiki itakayowawezesha wananchi wenye ulemavu wa miguu kupata huduma bila kikwazo.
Pia, Dkt. Mwanjelwa amesema, ofisi yake imedhamiria kuwa ya kwanza kutoa huduma katika mji wa serikali kama ilivyokuwa ya kwanza kuanza ujenzi katika mji huo, hivyo haoni kikwazo chochote cha kutekeleza azma hiyo kutokana na hatua nzuri ya ujenzi iliyofikiwa.
Ujenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika mji wa serikali, Ihumwa ni sehemu ya mwendelezo wa utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ya kuhamishia shughuli za serikali jijini Dodoma aliyoyatoa tarehe 25 Julai, 2016 wakati wa maadhimisho ya Kumbukumbu ya Siku ya Mashujaa.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) akiwa na Naibu Waziri, Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary
Mwanjelwa (Mb) na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais-Utumishi
wakiwasili katika Mji wa Serikali kuangalia maendeleo ya ujenzi wa ofisi
ya Utumishi katika mji huo Ihumwa, jijini Dodoma.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) akitoa maelekezo kwa
Mhandisi, Lucas Lipambila (kushoto) wakati wa ziara ya kuangalia
maendeleo ya ujenzi wa ofisi ya Utumishi katika mji wa serikali Ihumwa,
jijini Dodoma. Katikati ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb).
Afisa
Tawala Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw.
Donald Bombo akisisitiza jambo kwa Mhandisi Lucas Lipambila (wa pili
kutoka kulia) baada ya kumalizika kwa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst)
George Mkuchika (Mb) ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa ofisi ya
Utumishi katika mji wa serikali Ihumwa, jijini Dodoma
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) akizungumza mara baada ya
kumaliza ziara yake ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa ofisi za
Utumishi katika mji wa serikali Ihumwa, jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na baadhi ya watumishi
kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
Naibu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akisisitiza jambo baada ya
kukamilika kwa ziara ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa ofisi za
Utumishi katika mji wa serikali Ihumwa, jijini Dodoma. Kulia ni Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb).
Muonekano
wa jengo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora linalojengwa katika mji wa serikali Ihumwa, jijini Dodoma
No comments:
Post a Comment