HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 14, 2018

TAASISI YA WAJIBU YAWANOA WANAHABARI JUU YA KUONGEZA UELEWA WA WANANCHI KUHUSIANA NA UWAJIBIKAJI NA UTAWALA BORA

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
TAASISI ya WAJIBU inayojishughulisha na uwajibikaji na utawala bora chini ya mkurugenzi mtendaji na mkaguzi mkuu mstaafu wa hesabu  za serikalini (CAG) Ludovick Utouh  imekutana na kufanya majadiliano wa na wadau wa tasnia ya ya habari na kujadili dhana nzima ya uwajibikaji na utawala bora na namna ya kuripoti na kuandika makala kuhusiana nayo.

Akisoma hotuba kwa niaba ya  Mkurugenzi mtendaji wa taasisi wa WAJIBU Ludovick Utouh Meneja wa utawala na fedha Jackson Mmary amesema kuwa mjadala huo ni kati ya taasisi hiyo  pamoja ma waandishi wa habari ili kuweza kujenga taifa na kuongeza uelewa wa wananchi juu ya dhana nzima ya uwajibikaji na  utawala bora nchini.

Ameeleza kuwa taasisi ya WAJIBU inaamini kuwa uwajibikaji na utawala bora kwa pamoja ni muhimu sana katika maendeleo ya taifa licha ya kutoelewaka kwa watanzania walio wengi na kwa namna moja au nyingine wadau mbalimbali wanatakiwa kushirikiana ili kuweza kuwafikia wananchi na kuhakikisha wanaelewa dhana hiyo ya uwajibikaji inaeleweka.

Pia amesema kuwa taasisi hiyo ya WAJIBU inapendekeza taaluma ya habari lazima iwajibike zaidi kwa umma wa watanzania kwa kuendelea kuripoti kuhusu mambo yote yaliyoripotiwa huko nyuma  yenye umuhimu mkubwa kwa maendeleo ya wananchi ikiwa ni pamoja na mengi yaliyofanywa na serikali.

Akieleza majukumu ya taasisi hiyo amesema Afisa utafiti wa taasisi hiyo Hassan Kisena amesema kuwa taasisi hiyo ya fikra ya uwajibikaji iliyoanzishwa mwaka 2015 ina majukumu mengi  kubwa ikiwa ni kuangalia uwepo wa usimamizi mzuri wa rasilimali za umma pamoja na kuandaa ripiti za uwajibikaji kwa lugha rahisi ya ueleweka kwa wananchi, kuandaa machapisho ya uwajibikaji kisekta kama vile elimu, afya na maji sambamba na  kutoa mafunzo kwa wabunge, madiwani, AZAKI na mashirika mbalimbali na kuandaa makongamano ya uwajibikaji vyuoni kuhusu masuala ya kupiga vita rushwa na ufisadi kwa vyuo vikuu nchini ili kuwajenga wanafunzi hao kukataa na kupinga vitendo vya rushwa.

Amesema kuwa taasisi hiyo inafanyia kazi mapendekezo mbalimbali yanayotolewa  katika ripoti mbalimbali zikiwemo za CAG, PPRA, TEIT na PCCB kwa kuyaweka kirahisi zaidi na kufanyiwa kazi na amehimiza kuwa wao kama Wajibu wanaamini kuwa taarifa yenye manufaa makubwa kwa jamii lazima iripotiwe mfululizo hadi jambo hilo litakapokwisha na baadaye matokeo ya jambo hilo kutolewa.

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi mkuu wa kitengo cha mawasiliano serikalini kutoka ofisi ya taifa ya ukaguzi (NAOT) Sarah Reuben amesema kuwa ofisi ya ukaguzi wa hesabu za serikali (CAG) iliyoanzishwa  kikatiba chini ya ibara ya 143 ya katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na  inazingatia na kusimamia uwajibikaji na uzingatiaji wa sheria na kuhakikisha watumishi wa umma wanatekeleza majukumu yao na hayo yoe ni kwa kushirikisha vyombo vya habari.


Bi. Sarah amesema kuwa ofisi ya Rais inayohusika na utumishi wa umma imetoa miongozo kwa ofisi za za serikali kuhusisha vtombo vya habari  katika utoaji wa ripoti mbalimbali na pia ofisi hiyo huandaa warsha mbalimbali kwa waandishi mbalimbali na mara zote mnyororo wa thamani wa ofisi hiyo hukamilika kukiwa na mhimili wa CAG, serikali, bunge, wadau wa CAG na vyombo vya habari.
 Meneja wa Fedha na Utawala kutoka Taasisi ya WAJIBU Jackson Mmary akisoma risala ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya WAJIBU Ludovick Utouh  wakati wa ufunguzi wa warsha ya Majadiliano kati ya WAJIBU na waandishi wa habari iliyofanyika leo katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.
 Meneja wa Utafiti na Miradi kutoka Taasisi ya WAJIBU, Moses Kimaro aikitolea ufafanuzi baadhi ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari katika warsha wa Majadiliano kati ya WAJIBU na waandishi wa habari uliyofanyika leo katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.
Kaimu mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini  kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Sarah Reuben akiwasilisha mada kuhusu kazi zinazofanywa na ofisi hiyo kwa waandishi pamoja na wadau wa habari kwenye warsha ya Majadiliano kati ya WAJIBU na waandishi wa habari iliyofanyika leo katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.
Afisa Utafiti kutoka taasisi ya WAJIBU,  Hassan Kisena akiwasilisha mada kuhusu historia ya kuanzishwa kwa taasisi hiyo kwa wadau wa habari waliofika kwenye warsha ya Majadiliano kati ya WAJIBU na waandishi wa habari iliyofanyika leo katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.

Mwandishi Mwandamizi Vicky Ntetema akitoa uzoefu wake mbele ya wanahabari kuhusiana na dhana nzima ya uwajibikaji na utawala bora katika mkutano uliowakutanisha waandishi wa habari na taasisi ya WAJIBU leo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada kwenye warsha ya Majadiliano kati ya WAJIBU na waandishi wa habari uliyofanyika leo katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad