HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, December 9, 2018

NMB YAKABIDHI MSAADA WA MADAWATI 52 MUHIMBILI

 Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd akimkabidhi madawati 52 Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. John Rwegasha kwa ajili ya wagonjwa na ndugu wa wagonjwa wanaofika kupatiwa matibabu hospitali hapo. Katikati ni Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akishuhudia tukio hilo. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura wa Muhimbili, Dkt. Juma Mfinanga. Msaada huo una thamani ya Tsh. 10 milioni.
 Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akikagua madawati hayo. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba wa Muhimbili, John Rwegasha, Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura wa Muhimbili, Dkt. Juma Mfinanga.
 Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza na waandishi wa habari kabla ya NMB kukabidhi msaada wa madawati hayo kwa uongozi wa Muhimbili.
 Mkazi wa Kurasini jijini Dar es Salaam, Mariam Shaban akiishukuru Muhimbili pamoja na NMB kwa kuwapatia madawati hayo ambayo watayatumia kusubiri ndugu na jamaa  wakati wakipatiwa matibabu na wataalam wa afya. Pia, Bi. Mariam amemweleza Naibu Waziri jinsi wataalam wa Muhimbili walivyompokea vizuri mgonjwa wake na kuanza kumpatia matibabu kwa wakati.
Dkt. Ndugulile akizungumzia huduma za afya zinazotolewa na Muhimbili baada ya kukagua madawati hayo leo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad