HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 6, 2018

JESHI LA POLISI LAMAKATA WATUHUMIWA 14 WA WEZI WA MAGARI, SILAHA AINA SHOTGUN NA BASTOLA, RISASI NANE NA MLIPUKO

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limefanikiwa kukamata silaha moja aina ya Short Gun, risasi nne za short gun na mlipuko moja uliotengenezwa kienyeji.


Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, LIBERATUS SABAS-DCP ametos taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, amesema Silaha hiyo ilikamatwa tarehe 25 Oktoba 2018 majira ya saa 21:30 huko maeneo ya Kijichi. Askari wakiwa doria waliitilia mashaka pikipiki iliyokuwa haina namba za usajili ikiendeshwa na kijana mmoja akiwa amewapakia wenzake wawili.

Vijana hao baada ya kutambua kuwa wanafuatiliwa na Polisi walianza kuwafyatulia risasi huku wakikimbia, ndipo askari walipojibu mapigo na kufanikiwa kumjeruhi kijana mmoja na kupelekea kufariki akiwa anapelekwa hospitali.

Kijana huyo alipekuliwa na kukutwa akiwa na silaha aina ya Shotgun iliyokatwa mtutu na kitako ikiwa na risasi nne pamoja na mlipuko mmoja.

Msako mkali unaendelea kuwasaka watuhumiwa wote waliotoroka ikiwa ni pamoja na wahalifu wengine wanaofanya matukio ya kihalifu kwa kutumia silaha za moto ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Katika tukio lingine, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam huko maeneo ya Kijichi limefanikiwa kukamata silaha ndogo bastola aina ya Star ambayo haikuwa na namba za usajili na risasi nne ndani ya magazine.

Katika tukio hilo lililotokea tarehe 1 Novemba 2018 majira ya saa 22:15 huko maeneo ya Kijichi Mgeninani askari wakiwa doria walitilia mashaka waendesha pikipiki yenye usajili wa namba MC 854 BBY aina ya TVS iliyokuwa ikiendeshwa na mtu mmoja huku akiwa amepakia watu wengine wawili. 

Askari walipowasimamisha watu hao walikataa kutii amri halali na ghafla watu hao walifyatua risasi hewani ndipo Polisi walijibu mapigo na kuwajeruhi majambazi hao ambao walifariki wakiwa wanapatiwa matibabu hospitalini.

Watu hao walipekuliwa na kukutwa na silaha hiyo.

Kukamatwa kwa mtandandao wa wizi wa magari

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watuhumiwa 14 kwa tuhuma za wizi wa magari.

Watuhumiwa hao wamekamatwa sehemu mbalimbali hapa jijini Dar es Salaam na mikoa mingine wakiwa na magari 7, Bajaji moja na pikipiki moja ya wizi vyote vimeibwa maeno mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam.

Watuhumiwa hao ni Luckman Ramadhani (36 , Ignasi Faustine (35), Ally Shaweji (30), Stephen Mwanzalima (43), Emmanuel Mabula (42), Dismas Mfoyi (32), Nyamuhanga Matiko (29), Freeman Paul (35), Ayubu Makame (41), Erasto Nyamboneke (35), Seleman Saidi (42), Dickson Mbembaji (32), Ally Rashidi (35) na Robert Nassoro (46)

Magari yaliyokamatwa ni T 162 BLW Toyota land Cruiser MALI YA UWT-TANZANIA, STL 6434 Toyota Land Cruise MALI YA WIZARA YA AFYA, T 855 DLE Toyota Harrier, T 199 DEU Toyota Noah, T 249 DLL Toyota IST, T 255 AJG Rav4 gari hii ILIIBIWA udsm IKIWA na namba T 271 DFF, T 556 DJQ Toyota Allion ,  MC 854 BYY pikipiki aina ya  TVS Honda , MC 639 BYA Bajaji

Aidha kuna magari zaidi ya manne ambayo yamekamatwa mikoani, na yako njiani yanaletwa hapa jijini Dar es salaam kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi.

Watuhumiwa wanahojiwa na watafikishwa mahamani kwa hatua zaidi. Jeshi la polisi linaendelea na msako mkali dhidi ya wezi wa magari na watuhumiwa wengine.

Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, LIBERATUS SABAS-DCP akizungumza na waandishi wa habari akizungumziwa kukamatwa kwa watuhumiwa 15 wa uhalifu wa wizi wa magari, silaha na mlipuko mmoja.

Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, LIBERATUS SABAS-DCP akionesha silaha zilizokamatwa katika matukio tofauti ya uhalifu.

Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, LIBERATUS SABAS-DCP  akionesha moja ya gari lililoibiwa mali ya Wizara ya Afya na kukamatwa Mikumi Mkoani Morogoro.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad