HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 4, 2018

TIGO FIESTA SUPA NYOTA YAVUMBUA VIPAJI MKOANI RUKWA

Majaji wa shindano la Fiesta Super Nyota 2018 mkoani Rukwa, wakiongozwa na Jaji Mkuu, Adam Mchomvu (mwenye miwani), wakijitambulisha mbele ya washiriki na wageni mbalimbali waliofika kushuhudia kupatikana wa nyota wapya wa muziki wa kizazi kipya. wengine toka kulia ni Afisa Michezo Manispaa ya Rukwa, Adam Evarist, Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Rukwa, Charles Kiheka na kushoto ni The Baton A ambaye alikuwa mshindi wa Tigo Fiesta Supa Nyota mwaka jana.
Washiriki wakiwa kwenye mchujo wa mwisho uliotoa washindi wawili ambao watapanda kwenye jukwaa la Tigo Fiesta kesho uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga na kupata mshindi mmoja.
Moja kati ya washindi wawili wa Tigo Fiesta Supa Nyota mkoani Rukwa, Robby Gitaa akionyesha uwezo wake wa kuimba na kupiga gitaa kwenye shindano la kutafuta vijana wenye vipaji vya muziki mkoani humo leo.
Moja kati ya washindi wawili wa Tigo Fiesta Supa Nyota mkoani Rukwa, Tigani Tozi akionyesha uwezo wake wa staili ya kufokafoka kwenye shindano la kutafuta vijana wenye vipaji vya muziki mkoani humo leo. 
Adam Mchomvu akiwa na washiriki waliopenya Tano Bora.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad