HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 4, 2018

HAFLA YA KITAALUMA,SHUKRANI NA PONGEZI YAFANA KATIKA SHULE YA SEKONDARI MZUMBE MOROGORO




Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly ambaye alikuwaMgeni Rasmi katika Hafla ya Kitaaluma iliyo ambatana na Shukrani pamoja pongezi kwa mwanafunzi Bora kitaifa kidato cha Sita Bw. Anthony Mulokozi katika Shule ya Sekondari ya Mzumbe, Morogoro akitoa hotuba yake ambapo alimpongeza Anthony Mulokozi kwa kufanya vizuri, pia aliwapongeza walimu kwa kuendelea kuwa na juhudi za kuwafundisha wanafunzi kwa bidii na mwisho alisema kuwa juhudi zote hizi za elimu bora zinatokana na Serikali kuamua kulipa swala la elimu kipaumbele zaidi.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mzumbe Bw. Wenceslaus Mushi akielezea malengo ya Hafla hiyo ambayo ilikuwa ni ya kitaaluma zaidi na licha ya kuipongeza na kutoa Shukurani kwa Serikali lakini pia alimpongeza Tanzania One Anthony Mulokozi kwa kuwa Mwanafunzi Bora kidato cha sita kwa mwaka 2018 pamoja na wanafunzi wengine wote waliofanya vizuri pia aliwapongeza walimu kwa kuendelea kuwa na bidii ya kuwafundisha wanafunzi kwa weredi.

Afisa Elimu wa Shule za Sekondari Wilaya ya Mvomero Bw. Omat Sanga akizungumza neno wakati wa hafla hiyo ya kitaaluma iliyo ambatana na kutoa shukrani pamoja na pongezi katika Shule ya Sekondari Mzumbe .

Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mzumbe Bi. Jema Kimillo akielezea namna shule ilivyoweza kufanya vizuri kuanzia mwaka 2015 mpaka 2018, aliongeza kuwa matarajio yao ya sasa ni shule hiyo kuja kuongoza kitaifa.





Mwanafunzi Bora aliyechukua nafasi ya kwanza Tanzania nzima kwa kufanya vizuri mtihani wa Kidato cha Sita Bw. Anthony Mulokozi 'Tanzania one' aliyemaliza elimu yake ya kidato cha sita katika Shule ya sekondari Mzumbe, akitoa neno la shukurani pamoja na kuwapa moyo wanafunzi wengine ambapo aliwashukuru Wazazi wake kwa malezi mazuri,walimu ambao walikuwa wakimfundisha shuleni hapo pamoja na wanafunzi ambao alikuwa anasoma nao kipindi chote alichokua shuleni hapo, aliwasihi wanafunzi kuwa na mshikamano kimasomo, kusoma kwa bidii na kujiwekea malengo ya kufanikiwa katika masomo.

Mwenyekiti wa Wazazi Shule ya Sekondari Mzumbe Bw. Isack Wella akitoa salamu za pongezi kwa niaba ya wazazi wote pamoja na kuipongeza Halmashauri ya Mvomero kwa kuendelea kufanya kazi nzuri hasa kwa upande wa taaluma, pia walitoa zawadi wa walimu na Mwanafunzi Bora kitaifa katika mtihani wa kidato cha Sita Anthony Mulokozi.

Bw. Thomas Msuka ambaye ni mjumbe wa Bodi ya Shule ya Sekondari akitoa salam za pongezi kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi.
Kaka Mkuuwa Shule ya Sekondari ya Mzumbe Jarvis Bashabula, (anayesoma karatasi) akisoma hotuba kwa niaba ya Serikali ya Wanafunzi.

Katibu wa wazazi ya Shule ya Sekondari Mzumbe akikabidhi zawadi ya Tsh.500,000 kwa walimu wa Shule ya sekondari Mzumbe na Tsh. 300,000 kwa mwanafunzi bora Tanzania nzima katika mtihani wa kidato cha sita Bw. Anthony Mulokozi kwa mgeni rasmi Mh. Mohamed Utaly Mkuu wa Wilaya ya Mvomero.

Mgeni rasmi Mh. Mohamed Utaly(wa pili kulia) Mkuu wa Wilaya ya Mvomero akimkabidhi zawadi ya Tsh. 500,000 Mkuu wa Shule Bw. Wenceslaus Mushi kwa niaba ya walimu shule ya sekondari Mzumbe

Mgeni rasmi Mh. Mohamed Utaly (kulia) Mkuu wa Wilaya ya Mvomero akimkabidhi zawadi ya Tsh 300,000 Anthony Mulokozi iliyotolewa na wazazi wa shule ya Sekondari Mzumbe.




Baba Mzazi wa Anthony Mulokozi Bw. Julius Karugendo ambaye ni Afisa Ugani Idara ya Mifugo (aliyesimama) akitoa neno la shukurani kwa walimu kuweza kumsaidia Anthony Mulokozi pamoja na kualikwa kufikika katika hafla hiyo.




Mama Mzazi wa Anthony Mulolozi Bi. Anjela Kervin (wa kati kati kushoto) akikabidhiwa zawadi na umoja wa kinamama walimu Shule ya Sekondari Mzumbe wakati wa hafla hiyo.




Baba Mzazi wa Anthony Mlokozi Bw. Julius Karugendo akikabidhi zawadi kwa Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly ambayo alitoa kiasi cha Tsh 100,000 fedha alizo uza Mbuzi wake kwa ajili ya kuwapa walimu kama shukurani.




Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mvomero Mh. florian Kyombo akitoa neno la shukurani na kuwapongeza walimu kufanya kazi nzuri ya kuwafundisha wanafunzi na kumsihi Anthony Mlokozi kuongeza bidii maana anapoenda atakuwa huru bila kuwa na msimamizi.




Mh. Diwani ya Kata ya Mzumbe Rahel Kingu akitoa neno la Shukurani




Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly ambaye alikuwaMgeni Rasmi katika Hafla ya Kitaaluma iliyofanyika katika shule ya Sekondari Mzumbe akizindua rasmi Chombo cha mawasiliano mtandaoni cha shule hiyo kinachoitwa School Management System ambayo itawawezesha wazazi,walimu, wanafunzi na watu wengine ambao watakuwa na vigezo kutumia mtandao huo, pia utakuwa na sehemu ya wanafunzi kuona matokeo yao, kufanya test, wazazi kuona maendeleo ya wanafunzi na ku chat na walimu moja kwa moja kwa kutumia hata na simu zao za kiganjani




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly akijisajili katika system hiyo.




Mmoja wa wanafunzi aliyewahi kusoma katika shule hiyo Bw. Lusajo Ndago akitoa zawadi kwa niaba ya wanafunzi waliowahi kusoma shuleni hapo.




Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly akikabidhi zawadi katika shule ya wasichana Kikewa ambayo kwa mara ya kwanza imepeleka msichana kujiunga katika kidato cha tano ambapo Justina alichukua zawadi ya Tsh 100,000 kwa niaba ya Dada yake Grace. (Zawadi za Mkurugenzi)




Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Nassoro Seif Bi. Hawa akipokea zawadi ya Ths 300,000 kwa niaba ya shule fedha iliyokabidhiwa na Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly. (Zawadi za Mkurugenzi)




Mkuu wa Shule ya Sekondari Kikeo akipokea kwa niaba ya shule hiyo kutoka kwa Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly. (Zawadi za Mkurugenzi)




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(wa pili kulia) akimkabidhi mwalimu Adam Kilamuya kwa kufanya vizuri katika Idara ya Masomo ya Hesabu Mwaka jana kidato cha kwanza mpaka cha nne tsh 300,000. (Zawadi za Mkurugenzi)




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(wa pili kulia) akimkabidhi mwalimu Said H. Mohamed kwa kufanya vizuri katika Idara ya Masomo ya Literature English kwa O Level ambapo mwaka jana walikuwa wa pili kitaifa kati ya shule 908 pia walipata zawadi ya Tsh 300,000. (Zawadi za Mkurugenzi)




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(wa pili kulia) akimkabidhi mwalimu Gozbert Rwegasila kwa kufanya vizuri katika Idara ya Masomo ya Hesabu kwa A Level (Basic Applied Mathematics) walikuwa wa pili kitaifa kati ya shule 512 ambapo walipewa tsh 300,000 (Zawadi za Mkurugenzi)




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(wa pili kulia) akimkabidhi mwalimu Lidya Rwegelela kwa kufanya vizuri katika Idara ya Masomo ya Civics A Level ambao walikuwa wa tatu kitaifa kati ya shule 367 (Zawadi za Mkurugenzi)




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(wa pili kulia) akimpa mkono Mkuu wa Idara ya Chemistry kwa kufanya vizuri katika Maonesho mbalimbali ya kitaaluma ambapo mshindi alikuwa ni kutoka somo la Chemistry waliopata zawadi ya Tsh 200,000




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(wa pili kulia) akimpa Mkono wa pongezi mkuu wa Idara ya Kiswahili Bi. Jema Kimillo kwa kufanya vizuri katika Maonesho mbalimbali ya kitaaluma ambapo mshindi wa pili alitoka idara ya Kiswahili walipata tsh 100,000




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo ya ramani ya shule ya Sekondari Mzumbe kutoka kwa mwanafunzi wa kidato cha nnne Julius Nyambi(aliyevaa Sweta) na aliyetengeneza eneo hilo ni Wallen Kibaden (aliyevaa shati jeupe) wa ambao walikuwa idara ta Geography




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka kwa mwanafunzi kidato cha tano Anastasius Mdaku kuhusiana na Atmosphere idara ya Geography.




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kuhusiana na Udongo kutoka kwa mwanafunzi wa kidato cha tano Juma Shelukindo




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kuhusiana na upimaji (survey) ambapo mwanafunzi wa kidato cha tano Matalu Lubango akionesha vifaa vilivyokuwa vikitumika zamani na kuomba sasa waendane na Teknolojia kwa kuwa na vifaa vya kisasa.




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka kwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza (aliyevaa shati jeupe) Daniel Gabriel akitoa maelezo kuhusiana na Solar system.




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka kwa mwanafunzi wa kidato cha tano Alaphat Juma akitoa maelezo juu ya Dunia ilivyo tokea.




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka kwa Michael Nsopela kidato chaine kuhusiana na utamaduni na teknolojia katika idara ya Civics.




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka kwa Lukas Amiri kuhusiana na utengenezaji wa sabuni, na kusema kuwa pamoja na kusoma lakini wanafundishwa kuwa wajasiliamali.




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka kwa mwanafunzi wa kidato cha pili Mchoraji namna anavyochora picha zake




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo ya chimbuko la Kiswahili




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka idara ya Physics




Wanafunzi wa Kidato cha kwanza katika idara ya Chemistry kushoto ni Derick Kano na Christopher Luvinga




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka idara ya Hesabu hapa wanaelezwa namna hesabu zilivyo za muhimu katika ujenzi.




Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh. Mohamed Utaly(aliye vaa Skafu) akipata maelekezo kutoka Idara ya Biolohgy.




Waliokaa mbele ni walimu pamoja na watumishi wengine wa Shule ya Sekondari Mzumbe






Wanafunzi wakiwa katika Hafla hiyo.


Picha zote na Fredy Njeje

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad