HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 4, 2018

Innocent Sammy Bingwa “88 Pool Commpetitions 2018”.


Meneja Rasilimali watu (HR) WA Kampuni ya kutengeneza meza za Pool ya KENICE, Fionce Halelwa(kushoto) akimkabidhi Kikombe na Meza ya mchezo wa Pool yenye thamani ya Shilingi milioni mbili, Innocent Sammy mara baada ya kuibuka bingwa kwenye mashindano ya Pool ya mchezaji mmoja mmoja (Singles) yaliyojukana kwa “88 Kenice Pool Competitations 2018” yaliyofanyika katika Ukumbi wa Meeda Sinza jijini Dar es Salaam. 

Meneja Rasilimali watu (HR) WA Kampuni ya kutengeneza meza za Pool ya KENICE, Fionce Halelwa(kushoto) akimkabidhi fimbo maalumu za kuchezea mchezo wa Pool na Meza ya mchezo wa Pool yenye thamani ya Shilingi milioni mbili, Innocent Sammy mara baada ya kuibuka bingwa kwenye mashindano ya Pool ya mchezaji mmoja mmoja (Singles) yaliyojukana kwa “88 Kenice Pool Competitations 2018” yaliyofanyika katika Ukumbi wa Meeda Sinza jijini Dar es Salaam.
Meneja Rasilimali watu (HR) WA Kampuni ya kutengeneza meza za Pool ya KENICE, Fionce Halelwa(kushoto) akimkabidhi pesa taslimu Shilingi laki moja, Patrick Nyangusi mara baada ya kuibuka shindig wa pili kwenye mashindano ya Pool ya mchezaji mmoja mmoja (Singles) yaliyojukana kwa “88 Kenice Pool Competitations 2018” yaliyofanyika katika Ukumbi wa Meeda Sinza jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu.
KAMPUNI ya Kenice Tanzania imemkabidhi rasmi Bingwa wa mashindano ya Pool ya siku kuu ya nane nane Kikombe na meza ya Pool yenye thamani ya Shilingi milioni mbili, Innocent Sammy yajulikanayo kama “88 Kenice Pool Competitions 2018” yaliyomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Meeda jijini Dar es Salaam.

Akikabidhi zawadi Meneja Rasilimali Watu(HR) wa Kampuni ya Kutengeneza Meza za Pool ya Kenice, Fionce Halelwa, alimpongeza bingwa na kumuomba akaitumie vyema meza hiyo kwanza kama kitega uchumi lakini pia kama kiwanja maalumu cha mazoezi kwake cha kufanya kipaji chake cha kucheza pool kukua zaidi.

Alisema Fionce, tunatambua unakabiliawa na mechi kubwa ya Kimataifa na mchezaji kutoka Afrika Kusini, basi meza hii ikakusaidie kujiandaa vyema na shindano hilo ili ushinde na kuipa sifa Nchi yako ya Tanzania

Fionce alisema Kampuni ya Kenice itaendelea kusapoti mchezo wa Pool Tanzania kwa kadri watakavyojaliwa lakini zaidi pale wachezaji watakapokuwa wanafanya vizuri zaidi kwa ni hiyo ni hamasa pekee ya wao kuendelea kusaidia kwenye mchezo wa Pool.

Nae mratibu wa wa mashindano ya Pool, Michael machella alisema mashindano ya mwaka huu yalikuwa na hamasa ya pekee kwani yalishirikisha Wilaya tano za Mkoa wa Dar es Salaam kwa kipengele cha mchezaji mmoja mmoja(Singles) mpaka kumpata Bingwa wa mwaka huu 2018, Innocent Sammy

Machellah alisema ni mwaka wan ne sasa mfululizo akiandaa mashndano hayo na kila mwaka kampuni ya Kenice wamekuwa wakitoa ufadhili hivyo aliwashukuru sana kwa moyo wao huo na kuwaomba wasichoke kuisaidia Pool kwani mchango wao unatambulika kwa wachezaji na jamii ya Watanzani kwa ujumla.

Mwisho aliwapongeza washindi akianzia na Bingwa wa 2018, Innocent Sammy na mshindi wa pili Patrick Nyangusi ambao aliwataka wajiandae vyema na mashindano ya Kimataifa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad