HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 4, 2018

DKT MENGI ATEULIWA KUWA MLEZI WA SERENGETI BOYS

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF)leo Jumanne Septemba 4,2018 limemtangaza Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Dkt Reginald Mengi kuwa mlezi wa timu ya Taifa ya Vijana U17 "Serengeti Boys"


Dkt Mengi amekuwa akiifuatilia kwa karibu timu hiyo na amekuwa mmoja wa wadau wakubwa wa soka la Vijana.  Akiwa ni mpenda maendeleo ya mpira wa Miguu hususani soka la Vijana na amekuwa shabiki mkubwa wa Serengeti Boys.

TFF tunaamini tutashirikiana vizuri na Dkt  Mengi katika maendeleo na ustawi wa soka la Vijana na ni mwanamichezo ambaye hakika amekuwa mstari wa mbele katika kukuza na kuendeleza soka la Vijana. 

Mara kadhaa amekuwa akiwasiliana na TFF kufuatilia maendeleo ya timu ya Taifa ya U17 kwenye mashindano mbalimbali. 

TFF wamefarijika kwa Dkt Mengi kukubali kuwa mlezi wa timu hii ya Serengeti Boys na wanaamini kwa pamoja wataifanya timu hii kuwa msingi mzuri katika maendeleo ya ustawi wa soka la Vijana. 


Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Ndugu Reginald Mengi 




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad