HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 4, 2018

MAMA AMMWAGIA MWANAYE MAFUTA YA TAA NA KUMCHOMA MOTO

Mtoto wa Kike mwenye umiri wa miaka  13, (Jina limehifadhiwa) ameunguzwa baada ya kumwagiwa mafuta ya taa na  kisha kuwashwa na kiberiti na mama yake mzazi.

Binti huyo amelazwa katika hosptali ya St, Joseph Mbweni katika wodi ya watoto akiwa hawezi hata kutoa maelezo  vizuri.

Akizungumza jinsi mtoto huyo alivyofikishwa hospitalini hapo, Dkt,  Valentino Francis Bangi amesema, mtoto alifikishwa hospitalini hapo alfajiri ya Agosti 31 kuamkia Septemba Mosi mwaka huu akiwa katika hali mbaya, alikuwa ameunguzwa na moto sehemu ya mbele ya  kifua na usoni.

Dkt, Bangi amesema, mtoto huyo alipofikishwa hospitalini hapo alikuwa hawezi kupumua wala kuongea, lakini walimpatia huduma ya kumuweka katika hali nzuri na kuanza kurudi katika hali ya ubinadamu .

Dkt. Bangi amesema moja ya huduma waliyoifanya ni kumuoongezea maji pamoja na kumpatia huduma nyingine ya kumfanya apumue.

‘kwa sasa hali ya mgonjwa, anaendelea vizuri tofauti na alivyokuwa kwa sababu alikuwa hawezi hata kuongea, lakini sasa hivi anazungumza ambapo amelazwa wodi ya watoto hospitalini hapa.


Kwa upande wake, Ofisa Ustawi wa Jamii, wa Hospitali hiyo,  Angela Isingo ambaye anashughulikia masuala ya watoto, amesema tukio hilo linasikitisha , kwani wamemuhoji  binti huyo amesema aliyemfanyia kitendo hicho ni mama yake mzazi.

Isingo amesema mtoto huyo ameeleza chanzo cha tukio hilo kwamba, “binti alirudi usiku kutoka shule, mama yake akamuuliza kibubu cha pesa kiko wapi?, kwa sababu ndani kulikuwa na vibubu viwili havionekani kwa hiyo akaenda moja kwa moja kwa huyo mtoto na kumuuliza, anasema mtoto alimjibu kuwa hafahamu kibubu kilipo, mama yake akaendelea kumuhoji tena kuwa akitafute hadi akipate, akasema akazunguka akapata kibubu kimoja, na pale  ndani haishi peke yake ana baba yake na  ndugu zake wawili na dada yake mkubwa mmoja.

Akasema licha ya kumjibu mama yake kuwa hafahamu kibubu hicho kilipo, mama yake akaendelea kumuhoji kuwa, lazima aseme kibubu kilipokwenda ndiyo mama yake akachukua mafuta ya taa akamwagia na  kisha  akachukua kiberiti kumuwasha.

Amesema, baada ya kumuwasha ndiyo alihisi maumivu.

Hata hivyo, Isingo amesema, hali ya binti huyo ni nzuri kwa sasa tofauti na mwanzo alivyofikishwa hospitalini hapo alikuwa amevimba kwani kwa sasa maumivu ya ndani yamepungua. 

"Kitendo alichofanyiwa mtoto huyu cha kinyama na cha kikatili sana, nina amini vyombo vya dola vitafanya kazi yake kama nilivyosikia mama yake yupo polisi.

"Ninaamini sheria itashika mkondo wake na mimi nitasimamia kesi hii hadi inafika mahakamani, kwa sababu kesi nyingi za watoto huwa zinaishia njiani wanasema familia ikakae ielewane," amesema Isingo 

Ofisa huyo alisema lazima wasimame kidete kuhakikisha jambo hilo linakomoshwa na anaweza huyu akawa mfano kwa wamama wengine ambao wanawafanyia watoto wao au watoto wa kuwalea.tuwe walinzi wa watoto na si wa kuwafanyia vitendo vya kikatili.

Blogu ya jamii imefanikiwa kufika nyumbani kwa binti huyo na kufanikiwa kuzungumza na mdogo wa binti aliyechomwa moto (jina limehifadhiwa), anayesoma darasa la tatu hapa jijini, 

Akisimulia mtoto huyo ambaye ndiye aliyekuwa ameachiwa nyumba bada ya dada yake mkumbwa kwenda kupeleka chakuila Hospitali amesema, 
“Mama ndiyo alinituma nikanunue mafuta ya taa ya sh 300 pale dukani, (akionyeshea kwa kidole duka hilo), amesema, hakujua mama yake alitaka kufanyia nini mafuta yale, kwa usiku huo.

Alipoulizwa na Diwani wa kata ya bunju  mahali alipo mama yake, amesema, “mama yupo polisi na dada Angel ameenda hospitali kumpelekwa mgonjwa chakula (dada yake).

Amesema,mgonjwa aliunguzwa na mama,sababu alikuwa anachukua hela za mama ndani anaenda kuzila. Amesema wakati dada yake anachomwa yeye na mdogo wake walikuwa humo humo ndani lakini dada yao mkubwa Angel alikuwa nje, 

“Mama  alimuunguzia ndani sisi tukiwa humo humo tulipiga kelele. Nikamshuhudia dada anawaka moto kifuani, wakati huo baba hakuwepo,,baba alipokuja alimkuta Dada yupo ndani hajapelekwa hospitali, baba akauliza mama yake huko kuna nini, hapo sasa sijui mama alimjibuje baba. Tupo watoto wa nne dada Mary ni wa pili.

Amesema,baadae mama yao alimmwagia maji dada yake na kumzima moto ule sisi hatujafurahishwa na kitendo alichokifanya mama.Mama” amesimulia mtoto huyo.

Kwa upande wake, Alex John, Mjumbe na Katibu wa Shina namba tatu, kata ya bunju, ameelezea  tukio hilo la kusikitisha 

Amesema, aliamshwa majira ya saa tano kasoro usiku na dada mmoja ambaye ni jirani yake, aliyemtaja kwa jina la Maria Clement, amesema alimueleza kuwa jirani yangu kamuunguza mtoto na wanapiga makelele 

Nilipopata hiyo taarifa tukaongozana hadi nyumbani kwa mtoto huyo, bahati nzuri tukamkuta mama yake yupo, mume wake na watu wengine nikamuuliza kulikoni? Nipewa taarifa na jirani yenu kuwa mtoto wenu ameungua moto na nyinyi ndio mmemuunguza, wakaniambia kuwa yule ni mwizi.

Ameongeza, Nikawaambia hata kama ni mwizi yuko wapi? Sasa wakati wanataka kunipa maelezo ya kina akaja jirani yangu ambaye ni Abiti Njau akasema kuna nini mbona yule mtoto ameungua namna ile, nikamuuliza yuko wapi? akasema yupo kule kwangu Yale mazungumzo yakaishia pale, kwa hiyo sikupewa maelezo ya kina 

Ikabidi kuongozana na yule jirani yangu ili tuweze kumuona huyo mtoto kuona jinsi gani ambayo tunaweza kumsaidia, tulipofika tukaambiwa tena amekwenda bondeni kwa sababu alikuwa anapiga makelele huku analalamika, yaani alikuwa kama vile ukimchinja kuku halafu ukamuachia si anaweza akakimbia basi ndiyo kitu ambacho kilimtokea huyo mtoto

Wakati tunarudi tena eneo la tukio tukakuta wamemkata. “Kwa kweli nilivyomuona nilihisi kuumia sana, mtoto alikuwa ameungua kupita kiasi. Ili tukio kwa mujibu niliyopewa na dada Maria aliniambia mama mtu ndiye aliyehusika, muda huo sikujua baba mtu yuko wapi. Tulifanya utaratibu na kumpeleka mtoto hospitali baada ya kupata Fomu namba Tatu ya Polisi (PF3) kutoka polisi Mbweni.

Nilipowaeleza watoto kuhusiana na tukio hilo wakataharuki baada ya kumuona mtoto alivyounguzwa ,wakaniuliza nani alifanya hivyo, nikamwambia kwa taarifa ambazo ninazo Mimi hadi sasa mama yake ndiyo alimfanyia kitendo hiki, askari wakamchukua huyo mama wakamuweka chini ya ulinzi wakamuingia ndani.


Akizungumzia suala la baba wa mtoto huyo kuwa ana undugu na mkubwa mmoja wa Jeshi la Polisi kutaka kumaliza suala hilo mezani, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Bunju, Ibrahimu Mabeo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya usalama amesema wamesikia kuwa baba wa mtoto yupo uraiani, wataenda polisi yeye pamoja na Diwani kuhakikisha na baba mtu naye anachukuliwa hatua kwa sababu kama na baba naye anatetea jambo hilo la kinyama basi kama viongozi wa kata hatuwezi kulifumbia macho. 

Nae Diwani wa kata hiyo, Elly Nassoro ameeleza kusikitishwa kwake na tukio hilo, kwani kitendo kilichofanywa na  wazazi wa binti huyo ni cha aibu na kibaya. 

“Binti ameungua sana hali yake hatujui itakuwaje tunaomba Mwenyezi Mungu amsaidie ili apone. Kitendo ni cha kinyama kama tulivyomuhoji mtoto akasema mama ndiyo alimtuma kununua mafuta, halafu akachukua kiberiti akamuwasha”.

"Tumefikia hivi Watanzania kweli, kwa kweli inasikitisha sana wito wangu tuzidi kukemea maovu haya ambayo ya anaendelea kutokea kama vile mzazi mwenyewe anaweza kufanya hivi ni jambo la kutisha, tubadilishe," alisema Msingi 

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni , Murilo Jumanne Murilo amedhibitisha kutokea tukio hilo ambapo mama wa mtoto huyo wanamshikilia na wakati wowote watampandisha mahakamani.
“Taarifa hii ni ya kwali na mhusika tumeshamkamata na tumemuweka mahabusu na wakati wowote atapandishwa mahakamani kwa tuhuma hizo”amesema Murilo  
 Mtoto wa Kike mwenye umiri wa miaka  13, (Jina limehifadhiwa )ameunguzwa baada ya kumwagiwa mafuta ya taa na  kisha kuwashwa na kiberiti na mama yake mzazi.

Binti huyo amelazwa katika hosptali ya St, Joseph Mbweni katika wodi ya watoto akiwa hawezi hata kutoa maelezo  vizuri.

Akizungumza jinsi mtoto huyo alivyofikishwa hospitalini hapo, Dkt,  Valentino Francis Bangi amesema, mtoto alifikishwa hospitalini hapo alfajiri ya Agosti 31 kuamkia Septemba Mosi mwaka huu akiwa katika hali mbaya, alikuwa ameunguzwa na moto sehemu ya mbele ya  kifua na usoni.

Dkt, Bangi amesema, mtoto huyo alipofikishwa hospitalini hapo alikuwa hawezi kupumua wala kuongea, lakini walimpatia huduma ya kumuweka katika hali nzuri na kuanza kurudi katika hali ya ubinadamu .

Dkt. Bangi amesema moja ya huduma waliyoifanya ni kumuoongezea maji pamoja na kumpatia huduma nyingine ya kumfanya apumue.

‘kwa sasa hali ya mgonjwa, anaendelea vizuri tofauti na alivyokuwa kwa sababu alikuwa hawezi hata kuongea, lakini sasa hivi anazungumza ambapo amelazwa wodi ya watoto hospitalini hapa.


Kwa upande wake, Ofisa Ustawi wa Jamii, wa Hospitali hiyo,  Angela Isingo ambaye anashughulikia masuala ya watoto, amesema tukio hilo linasikitisha , kwani wamemuhoji  binti huyo amesema aliyemfanyia kitendo hicho ni mama yake mzazi.

Isingo amesema mtoto huyo ameeleza chanzo cha tukio hilo kwamba, “binti alirudi usiku kutoka shule, mama yake akamuuliza kibubu cha pesa kiko wapi?, kwa sababu ndani kulikuwa na vibubu viwili havionekani kwa hiyo akaenda moja kwa moja kwa huyo mtoto na kumuuliza, anasema mtoto alimjibu kuwa hafahamu kibubu kilipo, mama yake akaendelea kumuhoji tena kuwa akitafute hadi akipate, akasema akazunguka akapata kibubu kimoja, na pale  ndani haishi peke yake ana baba yake na  ndugu zake wawili na dada yake mkubwa mmoja.

Akasema licha ya kumjibu mama yake kuwa hafahamu kibubu hicho kilipo, mama yake akaendelea kumuhoji kuwa, lazima aseme kibubu kilipokwenda ndiyo mama yake akachukua mafuta ya taa akamwagia na  kisha  akachukua kiberiti kumuwasha.

Amesema, baada ya kumuwasha ndiyo alihisi maumivu.

Hata hivyo, Isingo amesema, hali ya binti huyo ni nzuri kwa sasa tofauti na mwanzo alivyofikishwa hospitalini hapo alikuwa amevimba kwani kwa sasa maumivu ya ndani yamepungua. 

"Kitendo alichofanyiwa mtoto huyu cha kinyama na cha kikatili sana, nina amini vyombo vya dola vitafanya kazi yake kama nilivyosikia mama yake yupo polisi.

"Ninaamini sheria itashika mkondo wake na mimi nitasimamia kesi hii hadi inafika mahakamani, kwa sababu kesi nyingi za watoto huwa zinaishia njiani wanasema familia ikakae ielewane," amesema Isingo 

Ofisa huyo alisema lazima wasimame kidete kuhakikisha jambo hilo linakomoshwa na anaweza huyu akawa mfano kwa wamama wengine ambao wanawafanyia watoto wao au watoto wa kuwalea.tuwe walinzi wa watoto na si wa kuwafanyia vitendo vya kikatili.

Blogu ya jamii imefanikiwa kufika nyumbani kwa binti huyo na kufanikiwa kuzungumza na mdogo wa binti aliyechomwa moto (jina limehifadhiwa), anayesoma darasa la tatu hapa jijini, 

Akisimulia mtoto huyo ambaye ndiye aliyekuwa ameachiwa nyumba bada ya dada yake mkumbwa kwenda kupeleka chakuila Hospitali amesema, 
“Mama ndiyo alinituma nikanunue mafuta ya taa ya sh 300 pale dukani, (akionyeshea kwa kidole duka hilo), amesema, hakujua mama yake alitaka kufanyia nini mafuta yale, kwa usiku huo.

Alipoulizwa na Diwani wa kata ya bunju  mahali alipo mama yake, amesema, “mama yupo polisi na dada Angel ameenda hospitali kumpelekwa mgonjwa chakula (dada yake).

Amesema,mgonjwa aliunguzwa na mama,sababu alikuwa anachukua hela za mama ndani anaenda kuzila. Amesema wakati dada yake anachomwa yeye na mdogo wake walikuwa humo humo ndani lakini dada yao mkubwa Angel alikuwa nje, 

“Mama  alimuunguzia ndani sisi tukiwa humo humo tulipiga kelele. Nikamshuhudia dada anawaka moto kifuani, wakati huo baba hakuwepo,,baba alipokuja alimkuta Dada yupo ndani hajapelekwa hospitali, baba akauliza mama yake huko kuna nini, hapo sasa sijui mama alimjibuje baba. Tupo watoto wa nne dada Mary ni wa pili.

Amesema,baadae mama yao alimmwagia maji dada yake na kumzima moto ule sisi hatujafurahishwa na kitendo alichokifanya mama.Mama” amesimulia mtoto huyo.

Kwa upande wake, Alex John, Mjumbe na Katibu wa Shina namba tatu, kata ya bunju, ameelezea  tukio hilo la kusikitisha 

Amesema, aliamshwa majira ya saa tano kasoro usiku na dada mmoja ambaye ni jirani yake, aliyemtaja kwa jina la Maria Clement, amesema alimueleza kuwa jirani yangu kamuunguza mtoto na wanapiga makelele 

Nilipopata hiyo taarifa tukaongozana hadi nyumbani kwa mtoto huyo, bahati nzuri tukamkuta mama yake yupo, mume wake na watu wengine nikamuuliza kulikoni? Nipewa taarifa na jirani yenu kuwa mtoto wenu ameungua moto na nyinyi ndio mmemuunguza, wakaniambia kuwa yule ni mwizi.

Ameongeza, Nikawaambia hata kama ni mwizi yuko wapi? Sasa wakati wanataka kunipa maelezo ya kina akaja jirani yangu ambaye ni Abiti Njau akasema kuna nini mbona yule mtoto ameungua namna ile, nikamuuliza yuko wapi? akasema yupo kule kwangu Yale mazungumzo yakaishia pale, kwa hiyo sikupewa maelezo ya kina 

Ikabidi kuongozana na yule jirani yangu ili tuweze kumuona huyo mtoto kuona jinsi gani ambayo tunaweza kumsaidia, tulipofika tukaambiwa tena amekwenda bondeni kwa sababu alikuwa anapiga makelele huku analalamika, yaani alikuwa kama vile ukimchinja kuku halafu ukamuachia si anaweza akakimbia basi ndiyo kitu ambacho kilimtokea huyo mtoto

Wakati tunarudi tena eneo la tukio tukakuta wamemkata. “Kwa kweli nilivyomuona nilihisi kuumia sana, mtoto alikuwa ameungua kupita kiasi. Ili tukio kwa mujibu niliyopewa na dada Maria aliniambia mama mtu ndiye aliyehusika, muda huo sikujua baba mtu yuko wapi. Tulifanya utaratibu na kumpeleka mtoto hospitali baada ya kupata Fomu namba Tatu ya Polisi (PF3) kutoka polisi Mbweni.

Nilipowaeleza watoto kuhusiana na tukio hilo wakataharuki baada ya kumuona mtoto alivyounguzwa ,wakaniuliza nani alifanya hivyo, nikamwambia kwa taarifa ambazo ninazo Mimi hadi sasa mama yake ndiyo alimfanyia kitendo hiki, askari wakamchukua huyo mama wakamuweka chini ya ulinzi wakamuingia ndani.

Akizungumzia suala la baba wa mtoto huyo kuwa ana undugu na mkubwa mmoja wa Jeshi la Polisi kutaka kumaliza suala hilo mezani, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Bunju, Ibrahimu Mabeo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya usalama amesema wamesikia kuwa baba wa mtoto yupo uraiani, wataenda polisi yeye pamoja na Diwani kuhakikisha na baba mtu naye anachukuliwa hatua kwa sababu kama na baba naye anatetea jambo hilo la kinyama basi kama viongozi wa kata hatuwezi kulifumbia macho. 

Nae Diwani wa kata hiyo, Elly Nassoro ameeleza kusikitishwa kwake na tukio hilo, kwani kitendo kilichofanywa na  wazazi wa binti huyo ni cha aibu na kibaya. 

“Binti ameungua sana hali yake hatujui itakuwaje tunaomba Mwenyezi Mungu amsaidie ili apone. Kitendo ni cha kinyama kama tulivyomuhoji mtoto akasema mama ndiyo alimtuma kununua mafuta, halafu akachukua kiberiti akamuwasha”.

"Tumefikia hivi Watanzania kweli, kwa kweli inasikitisha sana wito wangu tuzidi kukemea maovu haya ambayo ya anaendelea kutokea kama vile mzazi mwenyewe anaweza kufanya hivi ni jambo la kutisha, tubadilishe," alisema Msingi 

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni , Murilo Jumanne Murilo amedhibitisha kutokea tukio hilo ambapo mama wa mtoto huyo wanamshikilia na wakati wowote watampandisha mahakamani.
“Taarifa hii ni ya kwali na mhusika tumeshamkamata na tumemuweka mahabusu na wakati wowote atapandishwa mahakamani kwa tuhuma hizo”amesema Murilo

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad