HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, September 11, 2011

Salam za Rambirambi Kutoka Kwa Watanzania Waishio Atlanta


Watanzania tunaoishi katika jiji la Atlanta na vitongoji vyake tumeshtushwa, tumehuzunika na tumesikitishwa mno na taarifa za ajali ya meli ya Spice Islander iliyotokea September 10 2011.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu awalaze peponi wale wote waliofariki na tunawaombea wafiwa subra katika kipindi hiki kigumu.

Tunawashukuru sana wale wote waliofanya kazi ya kuokoa maisha na kusaidia kwa namna moja ama nyingine katika janga hili.

Halikadhalika, tunamshukuru sana Rais Jakaya Kikwete kwa kukatisha safari yake ya nje ya nchi kwa ajili ya kushughulikia janga hili. Pia tunamshukuru Dr. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania kuwa mstari wa mbele katika kuwafariji wafiwa.

Kwa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais Wa Zanzibar Maalim Seif, Makamu wa Pili wa Rais Wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na viongozi wengine wa Zanzibar, Inshallah mwenyezi Mungu atawasaidia katika kuukabili mtihani huu.

Inna Lillahi wa Inna Ilaihi Raajiun.

Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea.

John Kazilo

Rais wa Jumuiya ya Watanzania Waishio Atlanta 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad