Vijana
wa Kitanzania waishio Ugiriki wanatoa salam za rambi rambi kwa
watanzania wote hususan wazanzibari wa mkoa wa nungwi kufuatia janga la
kuzama kwa meli ya abiria.
Baada
ya kuwapa Pole tunapenda kutoa masikitiko yetu kwa watanzania
waliochukulia janga hili kama ni jambo jepesi tu,Ajali hii ilitokea
mnamo majira ya sa tisa za usiku na habari zilianza kusambaa tokea
wakati huo kupitia mitandao mbali mbali lakini cha kusikitisha ni kuwa
hata televisheni ya taifa haikujali kabisa kufuatilia nakuwapa habari
watanzania kwa ujumla.
Kampeni
za uchaguzi huko ingunga zilianza bila kujali na kulikuwa na burudani
za kutosha ikiwemo dansa na wachekeshaji,Kampuni ya simu za mkononi
Vodacom iliendelea na shuhuli zake za uandaaji wa Miss.Tanzania bila
kujali nini kimewasibu ndugu zetu wa Kizanzibari ambao ni watanzania kwa
ujumla.
Nchi
nyingi zilizoendelea huandaa nambari maalum za simu kupiga bure kwa
waathirika au mwenye habari yoyote ya kusaidia kuokolewa miili au
majeruhi,cha kushangaza kampuni hizo hazijajihusisha kabisa.
Ingekua
ajali hii inatokea wakati mashindano ya miss Tanzania yanafanyika
kusingekuwa na lawama lakini mashindano yalifanyika usiku baada ya masaa
zaidi ya 14 kutokea ajali na kusambaa kwa kasi habari za ajali hizo.
Sifikiri nchi yoyote mfano UK wakiomboleza mabomu ya 7/7 ikawa Scotland wanacheza ngoma na London wanaomboleza!
Kwa
kweli tumesikitishwa sana na vitendo hivi,hii inaonesha dharau kubwa
kwa wawekezaji ambao wanajali maslahi yao tu na sio maslahi ya
wanaowatumikia.
Tanzania
ni taifa moja na sio kama vile shilingi moja yenye sehemu mbili mkia na
kichwa,Janga linapotokea kote basi ni la kitaifa tu haijalishi
limetokea sehemu gani.
Kwa
kumalizia tunapenda kumpongeza Rais Kikwete kwa kukatisha ziara zake
muhimu na kuweka kambi Zanzibar,vile vile pongezi kubwa kwa serikali ya
Zanzibar kwa jitihada za uokoaji wa hali ya juu na pia wafanya biashara
wenye vyombo vya usafiri kwa kujitolea bila kujali maslahi yao,Na pia
Wananchi wa kijiji cha nungwi kwa kujitolea masaa 24 kuokoa na kupokea
maiti na waliojeruhiwa.
Tunatoa
salam nyingi sana kwa Rais Dr.Shein,Makamo wa kwanza na wa Pili wa
rais,pia waziri wa nchi Mh Aboud kwa kuwa mstari wa mbele kushuhulikia
janga hili na kuwa pamoja na wanachi kwa kipindi chote hiki.Tembelea
website yetu kwa habari zaidi.http://www.tanzaniansingreece.org
Mungu ibariki Tanzania.
IT Manager
Abdul
No comments:
Post a Comment