HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 31, 2011

"Rekodi” ya shuffle yang’arisha tangazo la Vodacom



“Rekodi” ya shuffle yang’arisha tangazo la Vodacom

Kampuni ya Vodacom Tanzania imeanza kutoa matangazo mapya ya televisheni yanayoendana na azma yake ya kuleta mapinduzi katika sekta ya mawasiliano ya simu nchini baada ya kufanya mabadiliko ya rangi kutoka buluu kuwa nyekundu pamoja na nembo ya biashara.

Katika tangazo jipya la kampuni hiyo lililonza kurushwa hewani hivi karibuni na vituo mbalimbali vya televisheni nchini na kupatikana pia katika mitandao ya kijamii ya intaneti – blogs mapinduzi ya utayaraishaji na ubunifu katika matangazo ya biashara vinaonakana.

Aidha kivutio kikubwa katika tangazo hilo ni picha za tamasha la kipekee la uchezaji wa muziki maarufu wa kisauzi - Koito ambapo lililenga kuvunja rekodi ya dunia ya idadi ya watu waliojikusanya na kucheza muziki kwa pamoja kwa wakati mmoja.

Tamasha hilo la wazi la aina yake lililohudhuriwa na maelfu ya wananchi wa kada mbalimbali lilifanyika Februari mwaka huu katika fukwe ya bahari ya Hindi eneo la Kigamboni jijinjni Dar es salaam ambapo bila kujali wingi huo wote walijipanga katika mistari iliyounda msitari mirefu isiyonakifani na kucheza muziki wa Koito kwa pamoja.

Afisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania, Mwamvita Makamba, amesema kuanza kurushwa kwa tangazo hilo ni mwanzo wa utekelezaji wa azma ya Vodacom Tanzania kuleta mapinduzi ya jumla katika sekta ya mawasiliano ya simu za mkononi nchini yanayokidhi kubadilika kwa sura nzima ya Vodacom Tanzania.

Mwamvita amesema Vodacom Tanzania baada ya kufanya mabadiliko katika rangi na nembo yake ya biashara kinachofuata sasa ni kwa watumiaji wa huduma hizo kunufaika na mabadiliko hayo kuanzia ubora wa huduma na namna ya kufikishiwa ujumbe wa upatikanaji wa huduma hizo na njia mpjawapo ni matangazo ya biashara

“Ukiangalia tangazo letu jipya utaona ni jinsi gani mapinduzi makubwa ya ufikishaji ujumbe kwa wananchi yanavyoanza na hiyo ndio azma yetu kwa sasa wengi walikuwa wanajiuliza ni kwa vipi tumeamua kuwa na vibonzo katika matangazo yetu ile ni njia mojawapo lakini njia nyingi zaidi zeney ubunifu, uhalisia na ubora wa hali ya juu zinafuata na wadau wetu watazifurahia”alisema Mwamvita.

Alisema Vodacom Tanzania imejipanga kuhakikisha kila hatua inayoipiga kwa sasa inaendana na ujumbe wa mabadiliko yaliyofanyika hivi karibuni ndani ya kampuni hususan mabadiliko ya rangi.

Katika tangazo hilo jipya Vodacom Tanzania inawakumbusha wadau huduma mbalimbali inazozitoa kwa ubora wa hali ya juu ikiwemo sauti na data na jinsi huduma hizo zinavyounganisha jamii mbalimbali kwa wepesi,urahisi na uharaka zaidi ya mitandao minginenchini.

“Tumefurahi kwamba wadau wetu na wananchi kwa ujumla wamepokea mabadiliko yetu katika mtazamo mzuri na kwa furaha na Vodacom Tanzania kubakia kuwa mtandao chagua bora zaidi kwa kada zote nchini lakini kwetu tunatambua nini zaidi tunawaandalia kukidhi mahitaji yao katika ubowa wa hali ya juu na kadri ziku zinavyosonga mbele wataendelea kuwa watu wa kujivunia katika soko la huduma za simu za mkononi nchini”alisisitiza Mwamvita.

Mabadiliko ya rangi katika Vodacom Tanzania yana maana kubwa katika utoaji huduma za kampuni hiyo sokoni lengo kuu ni kuwafanya wateja wa kampuni hiyo kuwa katikati ya mipango yote ya kampuni pamoja na utekelezaji wake chini ya kauli mbiu ya Kazi ni kwako ikilenga kuwapa nguvu na mamlaka zaidi wateja katika kuchagua na kurahisisha maisha kupitia huduma za Vodacom.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad