HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, May 8, 2011

DR. BILAL AWASILI UTURUKI KUMWAKILISHA RAIS KATIKA MKUTANO WA UMOJA WA MATAIFA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Dkt. Mbaraka Lijohiy, baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Ataturk, Istanbul jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Msaidizi wa Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Modest Mero, baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Ataturk jijini Istambul jana. Makamu wa Rais yuko nchini Uturuki kumwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa Umoja wa Matifa unahusu maendeleo ya nchi maskini, Mkutano huo unaanza kesho na kumalizika Mei 13, 2011. Katikati ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Sundery baada ya Dkt. Bilal kuwasili mjini Istambul jana. Makamu wa Rais yuko nchini Uturuki kumwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa Umoja wa Matifa unahusu maendeleo ya nchi maskini, Mkutano huo unaanza kesho na kumalizika Mei 13, 2011. Kushoto ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal,akiongozana na mkewe Mama Zakhia Bilal na baadhi ya viongozi alioongozana nao baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa ndege wa Ataturk, Istanbul jana Mei 7, kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa 4 wa Umoja wa Mataifa kuhusu maendeleo ya nchi maskini.
Makamu wa Rais, akiwa katika picha ya pamoja na Dkt. Mbaraka Ljohiy, ambaye ni Mkurugenzi wa Plastic , Reconstructive, Esthetic Had and Microsurgeory (kulia) na mfanyabiashara aishie nchini Uturuki, Ally Kilumba baada ya kukutana nao jana alipowasili jijini Instanbul, kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa 4 wa Umoja wa Mataifa kuhusu maendeleo ya nchi maskini. Picha kwa hisani ya Ofisi ya Makamu wa Rais

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad