



Na Mwandishi Wetu.
Washindi saba kati ya 10 waliojishindia vitita vya shilingi milioni 10 kila mmoja katika promosheni ya ‘Siku ya uwezo’iliyochezeshwa na Kampuni ya Vodacom Tanzania, mwishoni mwa wiki wamekabidhiwa hundi zao, baada ya kushinda shindano hilo.
Shindano hilo lilichezeshwa Aprili 4 mwaka huu, huku likiwataka wateja wao watume ujumbe mfupi wa maneno kuzungumzia malengo yao, endapo watafanikiwa kushinda Sh Milioni 10.
Timu ya watendaji wa Vodacom Tanzania ikiongozwa na Meneja Udhamini na Matukio wa kampuni hiyo, Rukia Mtingwa, ilitembelea maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, ili kujionea mazingira wanayoishi wateja hao walioshinda fedha hizo.
Akizungumza na waandishi wa Habari, Rukia alisema kwamba ziara hiyo ya siku nzima, ililenga kujua mazingira wanayoishi wateja wao wote ikiwemo wale wa mikoani mara baada ya washindi hao kuingiziwa fedha zao kwenye akaunti zao za benki.
Alisema shindano la Siku ya Uwezo lilibuniwa ili kuleta changamoto na kutimiza malengo kwa wateja walioamua kujitolea na kushikiriki promosheni hiyo.
“Nimefurahi kuona mazingira tofauti ya wateja wetu ambao ni washindi wenye bahati ya Siku ya Uwezo ya Vodacom. Ni matarajio yangu washindi wetu watazitumia pesa hizi vizuri kama walivyoandika meseji zao, wakiainisha malengo yao endapo watafanikiwa kushinda,” alisema Mtingwa.
Washindi hao wenye bahati ni pamoja na Innocent Julius Tete (Mbezi Juu), Yuda Joseph Mang’anya (Kinondoni), Gaspary Kasimiry Kamina (Chang’ombe), Fadhiri Felix Gwabisaba (Yombo Kilakala), Kombo Ally Athuman (Kipunguni B Ukonga), Judith Peter Ruge (Mongolandege) na Ibrahimu Abdallah Msigwa (Mbagala).
Kampuni ya Simu ya Mikononi ya Vodacom Tanzania, imekuwa ikichezesha promosheni mbalimbali kwa nia ya kuwawezesha wateja wao. Kupitia promosheni hii ya Siku ya Uwezo Zaidi, jumla ya wateja 10, waliibuka na ushindi huo. Kati ya hao miongoni mwao saba walitokea jijini Dar es Salaam wakati wengini ni wa mikoa ya Mwanza na Dodoma.
Washindi saba kati ya 10 waliojishindia vitita vya shilingi milioni 10 kila mmoja katika promosheni ya ‘Siku ya uwezo’iliyochezeshwa na Kampuni ya Vodacom Tanzania, mwishoni mwa wiki wamekabidhiwa hundi zao, baada ya kushinda shindano hilo.
Shindano hilo lilichezeshwa Aprili 4 mwaka huu, huku likiwataka wateja wao watume ujumbe mfupi wa maneno kuzungumzia malengo yao, endapo watafanikiwa kushinda Sh Milioni 10.
Timu ya watendaji wa Vodacom Tanzania ikiongozwa na Meneja Udhamini na Matukio wa kampuni hiyo, Rukia Mtingwa, ilitembelea maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, ili kujionea mazingira wanayoishi wateja hao walioshinda fedha hizo.
Akizungumza na waandishi wa Habari, Rukia alisema kwamba ziara hiyo ya siku nzima, ililenga kujua mazingira wanayoishi wateja wao wote ikiwemo wale wa mikoani mara baada ya washindi hao kuingiziwa fedha zao kwenye akaunti zao za benki.
Alisema shindano la Siku ya Uwezo lilibuniwa ili kuleta changamoto na kutimiza malengo kwa wateja walioamua kujitolea na kushikiriki promosheni hiyo.
“Nimefurahi kuona mazingira tofauti ya wateja wetu ambao ni washindi wenye bahati ya Siku ya Uwezo ya Vodacom. Ni matarajio yangu washindi wetu watazitumia pesa hizi vizuri kama walivyoandika meseji zao, wakiainisha malengo yao endapo watafanikiwa kushinda,” alisema Mtingwa.
Washindi hao wenye bahati ni pamoja na Innocent Julius Tete (Mbezi Juu), Yuda Joseph Mang’anya (Kinondoni), Gaspary Kasimiry Kamina (Chang’ombe), Fadhiri Felix Gwabisaba (Yombo Kilakala), Kombo Ally Athuman (Kipunguni B Ukonga), Judith Peter Ruge (Mongolandege) na Ibrahimu Abdallah Msigwa (Mbagala).
Kampuni ya Simu ya Mikononi ya Vodacom Tanzania, imekuwa ikichezesha promosheni mbalimbali kwa nia ya kuwawezesha wateja wao. Kupitia promosheni hii ya Siku ya Uwezo Zaidi, jumla ya wateja 10, waliibuka na ushindi huo. Kati ya hao miongoni mwao saba walitokea jijini Dar es Salaam wakati wengini ni wa mikoa ya Mwanza na Dodoma.
No comments:
Post a Comment