Y9 Microfinance imezindua matawi mapya matano jijini Dar es Salaam ili kuimarisha utoaji wa huduma, huku ikilenga kuwafikia Watanzania wengi zaidi.
Matawi hayo yaliyopo
maeneo ya Makumbusho, Mbezi Luis, Tandika, Kigamboni na Buguruni
yatawezesha wateja kupata huduma za mikopo kwa urahisi zaidi.
Y9
imekusudia kuongeza urahisishaji kwa wateja ambao hawawezi kumudu
ununuzi wa mara moja wa simu janja na wanatafuta njia za mbadala za
mkopo wa simu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi
Mtendaji wa Y9, Faith Pella alisema hatua hiyo ni mkakati wake wa kukuza
biashara ya Y9 Microfinance kwa kupeleka huduma za mkopo wa simu janja
karibu na wateja wetu. Tunatoa huduma za mkopo wa simu janja za 4G kwa
vikundi tofauti wakiwemo wafanyakazi, wajasiriamali na watu binafsi.
“Tunafuraha
kuwataarifu wateja wetu kwamba, sasa wanaweza kupata huduma zetu kwa
urahisi katika vituo vyetu vya Y9 kote jijini Dar es Salaam na
tutaendelea kufungua katika mikoa mingi zaidi ili kuwafikia wateja wengi
zaidi nchini,” Mkurugenzi Mtendaji wa Y9 alisema.
Y9
kushirikiana na Samsung tunatoa simu mahiri za bei nafuu na zenye ubora
kwa Watanzania. Wateja sasa wanaweza kupata mkopo wa simu aina ya
Samsung kwa urahisi kwa bei ya chini ya kianzio ya TZS 40,000 kupitia Y9
Microfinance na kurejeshakuanzia TZS 2,000 kwa siku kama marejeshoya
mkopo, " Mkurugenzi Mtendaji wa Y9 aliongeza.
"Tumeanza na mkopo
wa simu janja, na tunamipango endelevu ya kuleta huduma zaidi ili
kuwapa wateja wetu huduma bora za kifedha zitakazopatikana katika
programu yetu ya Y9" aliendelea.
Y9 imejipanga kutoa
ushirikishwaji wa kifedha kupitia huduma za kifedha za kidijitali ambazo
zitaathiri maisha ya kijamii na kiuchumi ya watu wa Tanzania.
Kwa maelezo zaidi, mteja anaweza kupiga 0 800 75 0260 bila malipo na kupata maelezo zaidi kuhusu jinsi ya kupata huduma hii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Y9 Microfinance Faith
Pella akiwa sambamba na Mkuu wa Kitengo chaa Mauzo na Usambazaji
Fredrick Mtui wakikata utepe ikiwa ni moja ya uzinduzi wa matawi
mapya matano ya taasisi hiyo jijini Dar es Salaam, ili kuimarisha
utoaji wa huduma, huku ikilenga kuwafikia Watanzania wengi zaidi.
Wa tatu kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Y9 Microfinance Faith Pella alipokuwa akizungumza na Baadhi ya waandishi wa habari mara baada ya kuzindua moja ya tawi kati ya matawi
mapya matano ya taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam, ili kuimarisha
utoaji wa huduma, huku ikilenga kuwafikia Watanzania wengi zaidi.
Mkuu wa Kitengo chaa Mauzo na Usambazaji wa Y9 Microfinance ,Fredrick
Mtui akifafanua jambo kwa baadhi ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani)
mara baada ya kuzindua moja ya tawi kati ya matawi
mapya matano ya taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam, ili kuimarisha
utoaji wa huduma, huku ikilenga kuwafikia Watanzania wengi zaidi.
No comments:
Post a Comment