HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, August 3, 2022

UJUMBE WA BENKI YA DUNIA WAKAGUA MAENDELEO YA MRADI WA TANZANIA YA KIDIJITALI

Mratibu wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Honest Njau (kushoto) akizungumza na Bw. Xavier Daudi, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (katikati) na Kiongozi wa Ujumbe wa Benki ya Dunia Dkt. Tim Kelly wakati ujumbe wa Benki ya Dunia wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali walipotembelea na kufanya mazungumzo na watendaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Mulembwa Munaku akizungumza na Ujumbe wa Benki ya Dunia walipofika katika Ofisi za Wizara hiyo Agosti 2, 2022 na kufanya mazungumzo kuhusu maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali.

Mratibu wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Honest Njau (kushoto) akizungumza na Bw. Xavier Daudi, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (katikati) na Kiongozi wa Ujumbe wa Benki ya Dunia Dkt. Tim Kelly wakati ujumbe wa Benki ya Dunia wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali walipotembelea na kufanya mazungumzo na watendaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.



Matukio mbalimbali katika picha wakati wa ziara ya Ujumbe wa Benki ya Dunia katika ofisi za Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mamlaka ya Serikali Mtandao zilizopo jijini Dodoma kwa lengo la kutembelea na kufanya mazungumzo kuhusu maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Tanzania ya Kidijitali.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad