HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 8, 2022

Taasisi ya Dun & Bradstreet yazindua teknolojia mpya iitwayo EDX.

 


• Teknolojia hii ya EDX hurahisisha uchakataji na uwasilishaji wa taarifa za wakopaji kwa taasisi za kifedha kwa njia ya kielektroniki.


• Uwasilishaji wa taarifa za wakopaji kwa njia hii ya kisasa utarahisisha mtiririko wa kazi kwa taasisi husika, kupunguza makosa pamoja na kusaidia taasisi kufuata kanuni na sheria za Benki Kuu ya Tanzania za ukusanyaji wa taarifa za mikopo.

  Taasisi ya Dun & Bradstreet Bureau Tanzania ambayo ni kampuni tanzu ya Dun & Bradstreet Credit Bureau Limited, leo imetanganza kuzindua teknolojia mpya yenye uwezo mkubwa wa kuchakata, kusafirisha na kuwasilisha taarifa kwa haraka inayojulikana kama EDX. 

EDX ni maalum kwa taasisi za kifedha zinazotoa mikopo pamoja na uwasilishaji wa taarifa za wakopaji kwenda kwenye kanzi data ya Benki Kuu ya Tanzania. EDX itasaidia taasisi za kifedha kuondoa makosa wakati wa uwasilishaji wa taarifa hizo, kuokoa gharama pamoja na kutoa taarifa sahihi pale zinapohitajika.

EDX ni teknolojia ambayo hurahisisha uchakataji na uwasilishaji wa taarifa za wakopaji kwa taasisi za kifedha kwa njia ya kielektroniki. Vile vile, uwasilishaji wa taarifa za wakopaji kwa njia hii ya kisasa utarahisisha mtiririko wa kazi kwa taasisi husika, kupunguza makosa pamoja na kusaidia taasisi kufuata kanuni na sheria za Benki Kuu ya Tanzania za ukusanyaji wa taarifa za mikopo.


Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza uzinduzi wa EDX, Meneja wa taasisi ya Dun & Bradstreet Tanzania Junaid Malik alisema ‘Teknolojia ni moja ya nguzo kuu kwa taasisi za kifedha na benki. 

Hata hivyo, uwepo wa teknolojia hii katika sekta umesababisha kuongezeka kwa idadi ya taarifa zinazohifadhiwa, usimamizi wa taarifa pamoja na ongezeko la mahitaji ya taarifa kutoka kwa wasimamizi wa sekta ya fedha. EDX hurahisisha uchakataji wa taarifa kieletroniki ili taasisi za kifedha ziweze kuzituma katika mfumo unao stahili wakati wa upelekaji wa taarifa za wakopaji kwa kwa Benki Kuu ya Tanzania pale zinapohitajika”.


Malik aliongeza “Tumeweza kuweka mtiririko wa taarifa kuwa wa kieletroniki ili uwasilishaji wa taarifa kuwa wa kisasa, hakuna sababu ya kujiongezea gharama za teknolojia mfumo huu unakupa uhakika kwa kuzingatia vigezo na kanuni za ukusanyaji na uwasilishaji wa taarifa za mikopo kwa usahihi. Unaweza kutoa taarifa kutoka kwenye vyanzo tofauti ukaziweka pamoja kwa kufuata taratibu za biashara yako kisha ukaziweka kwenye muundo wowote unaotakiwa kulingana na kanuni na sheria za Benki Kuu ya Tanzania.

Wataalamu wa Dun & Bradsheet Credit Bureau Tanzania watasaidia kwenye uunganishaji wa EDX. Baada ya EDX kuunganishwa kwenye taasisi husika, mfumo huo utaendelea kufanya kazi kielektroniki.

EDX itahakikisha uwasilishaji wa taarifa kwa usahihi, kwenye muonekano mzuri kwa watumiaji na kutoa ripoti ya kina. Vipengele hivi hutoa uwezo kwa watumiaji kutathmini mtiririko mzima wa uwasilishaji wa taarifa pamoja na kurekebisha, kuthibitisha vyanzo vya taarifa hizo kwa kuzingatia uhitaji.

Malik alisema kuwa EDX inasaidia kuokoa gharama za uendeshaji kwa zaidi ya asilimia 75%, ni rahisi na haraka kuunganisha inachukua muda mfupi usiozidi wiki tatu huku miundombinu yake ikichukua nafasi ndogo zaidi kama teknolojia ya Kubernetes.

‘EDX pia inasaidia kufikia vyanzo vingi vya taarifa, kuwasilisha, kuhakiki na kuchapisha kwenye muundo wowote. Inapunguza uingizaji wa data kwa mkono kwa asilimia 90%, kutoa taarifa kwa wakati na kupunguza kupoteza muda kwa zaidi ya asilimia 85%’ alisema Malik.

EDX inapatikana kwa manunuzi kutoka Dun & Bradsheet Credit Bureau Tanzania. Kwa maelezo Zaidi wasiliana nasi kupitia namba +255 222 135 445.


 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad