Mkuu
wa Mkoa wa Tanga, Adam Malima amewataka madiwani wa Halmashauri ya
Wilaya ya Korogwe kuwa na mkakati wa pamoja kuokoa mapato katika
halmashauri hiyo.
Malima
amesema hayo jana wakati akizungumza katika Kikao cha Baraza la
Madiwani wa halmashauri hiyo cha kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) wilayani Korogwe.
“Ukitosheka
na kidogo kila siku unakuwa mdogo, madiwani tutamani vitu vikubwa na
sisi hapa dhahabu yetu ni mkonge tuitunze kama chanzo cha mapato. Mapato
yetu mwaka mzima Sh milioni 400 hamuoni haya, pambaneni halmashauri
yenu iwe na fedha.
“Nawasihi
madiwani kaeni kwenye nafasi ya kujielewa kuinusuru Korogwe, ukiangalia
hoja za CAG ziko 38, zote hizo za nini na katika hizo za msisitizo ziko
15 hii inamaanisha kuna kitu hakiko sawa.
“Nitamuita
mkurugenzi nitamuuliza kama ameshindwa kazi wala simsubiri Mheshimiwa
Rais aje kuniuliza kama nimeshindwa kazi nitatenda kabla sijaulizwa.
Matarajio yangu Korogwe Wilaya mtajipanga na mtakuja vizuri,” amesema
Malima.
Awali,
akizungumza katika kikao hicho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Pili
Mnyema alisema Halmashauri ya Korogwe ni moja ya halmashauri ambazo
zimekuwa hazifanyi vizuri hususani kwenye usimamizi wa miradi na
watendaji wake bado wanaendelea kufanya kazi kwa mazoea.
Alisema
Machi mwaka huu ilifanyika tathmini ya utendaji kazi kwa halmashauri
zote hapa nchini na katika mkoa wa Tanga kuna halmashauri tatu ambazo
utendaji wake ulionekana hauridhishi kulingana na vigezo
vilivyoainishwa na kubainisha kuwa miongoni mwa hizo Halmashauri ya
Korogwe Wilaya, Lushoto na Bumbuli na sababu ni hizo hizo usimamizi wa
miradi na mambo ya asilimia 10.
“Sasa
hapo waheshimiwa madiwani mtaona bado kuna watendaji ambao wanaendelea
kufanya kazi kwa mazoea kwa sababu hawatekelezi wajibu wao ipasavyo,
hawajali na mwisho wa siku wanasababisha halmashauri ya Wilaya ya
Korogwe iingie kwenye matatizo kwa ajili ya watendaji wachache ambao
mwaka 2020 wananchi waliwapa dhamana ya kusimamia halmashauri yao,”
alisema.
Pamoja
na mambo mengine, aliwataka madiwani kuona kwamba wao ni sehemu ya
kuhakikisha Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe inafanya vizuri ambapo pia
aliwataka kuripoti iwapo mtendaji anakwamisha miradi ya halmashauri
hiyo.
“Nawashauri
kusema kama mnaona kwamba huyu mtu anatukwaza na kuendelea kuwepo kwake
sisi hatutafanikiwa lakini mkikaa kimya na ninyi mnakuwa ni sehemu ya
hilo tatizo.
“Mkurugenzi
na wewe usicheke na hawa watendaji wanaolega lega, taratibu
zinakuruhusu kama mtumishi hawajibiki kwenye utumishi wa umma kama.
Tunataka mwakani tukija basi muwe sehemu ya kupongezwa kutoka kwenye
hali moja kuelekea nyingine," alisema.
No comments:
Post a Comment