HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 13, 2022

RAIS SAMIA AWASILI MUSCAT NCHINI OMAN KWA AJILI YA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TATU

 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama pamoja na Mwenyeji wake Kiongozi Mkuu wa Taifa la Omani Sultan Haitham bin Tariq Al Said wakati Wimbo wa Taifa wa Tanzania ukipigwa katika mapokezi Rasmi yaliyofanyika kwenye viwanja vya Kasri ya Al Alam Muscat nchini Oman tarehe 12 Juni, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyeji wake Kiongozi Mkuu wa Taifa la Omani Sultan Oman Haitham bin Tariq Al Said kabla ya kuanza mazungumzo yaliyofanyika Kasri ya Al Alam Muscat nchini Oman tarehe 12 Juni, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Oman mara baada ya kuwasili Kasri ya Al Alam Muscat nchini humo tarehe 12 Juni, 2022.
Kikosi cha Jeshi la Oman kikiwasili katika viwanja vya Kasri ya Al Alam kwa ajili ya Mapokezi Rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Muscat nchini Oman tarehe 12 Juni, 2022. PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad