Mwenyekiti
wa ACT Wazalendo Ndugu Juma Duni Haji ametoa rai kwa Kikosi Kazi cha
Rais cha Kuratibu Maoni ya Wadau Kuhusu Demokrasia kuzingatia matakwa ya
Wananchi na maoni ya wadau katika Ripoti yao.
Rai
hiyo imetolewa akiwahutubia Wanachama wa ACT Wazalendo katika Majimbo
ya Tunduru Kusini na Tunduru Kaskazini jana tarehe 19 Juni 2022.
"Nilipokutana
naye, nilimpongeza Mh. Rais Samia Suluhu kwa kuundwa kwa Kikosi Kazi
ambacho kinawajibika kwake moja kwa moja. ACT Wazalendo tumepeleka maoni
yetu ya kina kuhusu Tume Huru ya Uchaguzi, Katiba Mpya na maeneo
mengine. Tunatoa rai kwa Kikosi Kazi kuzingatia ipasavyo maoni
yaliyotolewa na wadau na kutanguliza mbele matakwa ya wananchi katika
kutekeleza majukumu yake na kuandika Ripoti yao"-alisema Ndugu Ado.
"Haipendezi
kuwa kila Uchaguzi ukija tunauwana na kuumizana. Nimemweleza Mh. Rais
tulikomeshe hili. Tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ili chaguzi zijazo
ziwe za haki, huru na zenye kuaminika"-alisisitiza Ndugu Duni.
Katika
hatua nyingine, Babu Duni aliwaeleza Wanachama wa ACT Wazalendo wa
Tunduru kuwa ACT Wazalendo itaendelea kuupinga mfumo wa stakabadhi
ghalani kwenye ununuzi wa mazao ya korosho, mbaazi, ufuta n.k kwa sababu
haujaweza kutatua changamoto za wakulima hasa kuhusu kulipwa bei nzuri
za mazao kwa wakati.
Pia,
Babu Duni alitoa nasaha kwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Ndugu Julius
Mtatiro kuzingatia haki za raia anapotekeleza majukumu yake.
"Mtatiro
ni kijana wetu. Tulimpokea na kumpa nafasi. Akiwa upinzani aliwahi kuwa
Mkurugenzi wa Haki za Binadamu. Naambiwa hivi sasa amebadilika na
anafikia hatua ya kutaka kuwafunga Wanawake wanaodai haki yao baada ya
kuondolewa kazini kwenye Kiwanda cha kubangua Korosho. Namuomba
abadilike na ajali haki"-Alihitimisha Babu Duni.
Mwenyekiti
wa Chama yupo kwenye ziara ya ujenzi wa Chama kwenye Mikoa ya Mkoa wa
Kichama wa Selous, Mtwara na Lindi kuanzia tarehe 19 hadi 21 Juni 2022.
Ameambatana na Katibu Mkuu Ado Shaibu na Mjumbe wa Kamati Kuu Isihaka
Mchinjita.
Akiwa
kwenye Majimbo ya Tunduru Kusini na Tunduru Kaskazini amekagua ujenzi
wa Ofisi ya Kata ya Ligoma na kuzindua ujenzi wa Ofisi ya Kata ya
Muhuwesi.
Janeth Rithe, Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, ACT Wazalendo.
20 Mei 2022.
No comments:
Post a Comment