HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 1, 2021

Tanzania katika mkutano 26 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea Glasgow

'
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akilakiwa na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo katika Mkutano 26 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea mjini Glasgow, Uingereza.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Dkt. Asha Rose Migiro akiteta jambo na ujumbe wa Tanzania katika mkutano 26 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea Glasgow, Uingereza. Kushoto ni Dkt. Andrew Komba Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Dkt. Asha Rose Migiro akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea Glasgow, Uingereza. Ujumbe huo ni kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na Benki ya CRDB.
Bi. Emelda Teikwa Afisa Mazingira Mkuu (aliekaa), Bi. Hadija Kayera (wa kwanza kushoto) Afisa Mazingira na Dkt. Emma Liwenga Msaidizi wa Makamu wa Rais (Mazingira) wakiwa katika Mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea Glasgow, Uingereza. Kulia ni Bi. Zaninabu Sheuya Afisa Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo.
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad