Dodoma, Tanzania.
Naibu
Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe amesema ya kuwa “Serikali ya
Tanzania imefanikiwa kufungua soko la parachichi nchini Afrika ya Kusini
baada ya muda mrefu wa majadiliano baina ya mamlaka za Afrika ya kusini
na Tanzania na kuhitimisha miaka kumi ya mgogoro wa zao la parachichi
uliokuwepo baina ya nchi hizi mbili”
Aidha, Mheshimiwa Bashe
ameyataja mafanikio haya kama hatua muhimu ya kulinda masoko ya mazao
yanayozalishwa nchini na kujenga ushirikiano mpya katika sekta ya Kilimo
ili kuhakikisha kunakuwa na ubora wa mazao pamoja na bidhaa zitokanazo
na kilimo ili kuleta tija ya kilimo miongoni mwa wakulima nchini.
Mafanikio
haya ya sasa yanakua ni sehemu Muhimu ya kumaliza sintofahamu
iliyotokea mapema mwezi Februari mwaka 2021 ambapo mamlaka za Afrika ya
kusini ziliharibu zaidi ya Tani 3 za parachichi ambazo zilisafirishwa
nchini humo na kampuni ya kitanzania ya Kuza. Hata hivyo tokea hapo
viongozi wa Wizara ya Kilimo, wataalamu wa Afya za mimea na taasisi za
udhibiti viwango na ubora za panda zote zimekuwa zikikutana ili kuwa na
makubaliano rafiki Kwa pande zote mbili.
Zao la parachichi ni
moja ya mazao Muhimu Kwa ajili ya sekta ya biashara nchini ambayo
imekuwa ikikua Kwa kasi. Uchunguzi kitakwimu unabainisha ya kuwa mnamo
mwaka 2012, kiasi cha mauzo ya nje ya zao la Parachichi yalifikia kilo
488,492, huku miaka mitatu baadae yaani mwaka 2015 Tanzania ilisafirisha
Kilo 2,579,976 Ikiwa ni ongezeko la 428.48%
Kwa mujibu wa
mtandao wa taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) mnamo mwaka 2018
pekee, Tanzania iliuza nje ya nchi jumla ya Tani 7,551 za parachichi
ambazo ziliingizia taifa fedha za kigeni zenye thamani ya Dola za
kimarekani milioni 8.5 ikiwa ni sehemu ya biashara Kwa nchi za mabara ya
Ulaya, Afrika na Asia huku bara la Ulaya pekee likiwa ni mnunuzi Mkuu
Kwa kutumia asilimia 85 ya parachichi zote zinazozalishwa nchini.
Kwa
mujibu wa Mtandao wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini; Tanzania ni
nchi ya Pili kwa uzalishaji wa zao la parachichi barani Afrika ikiwa
nyuma ya Kenya huku uzalishaji nchini Tanzania ukifikia tani 190,000 Kwa
mwaka
Monday, November 22, 2021

BASHE: TUMEFANIKIWA KUFUNGUA SOKO LA PARACHICHI NCHINI AFRIKA YA KUSINI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment