HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 16, 2021

RC KUNENGE AZINDUA MAGARI MAPYA YA HONG YANG KIBAHA MKAONI PWANI

 

  

 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amezindua awamu ya  pili ya utengenezaji wa magari aina ya HONG YANG katika kiwanda cha GF Assemblers Kibaha mkoni Pwani

Akizungumza baada ya uzinduzi wa magari hayo, Kunenge alikemea baadhi ya tabia za watendaji wa serikali za kupishana katika ofisi za wawekezaji kwa visingizio mbali mbali mbali

 Ikiwamo kulazimisha kuonana na wamiliki ama kwa visingizio vya kutaka kufanya ukaguzi  hali inayowafanya wawekezaji kuwa na hofu na kujikuta wanashindwa kutimiza majukumu yao

Kunenge alisema Serikali ya mkoa wa Pwani inahakikisha inapata maendeleo kwa kuongeza fursa ya biashara na uwekezaji wenye mazingira rafiki na utawala bora kwa hiyo hataki kusikia ama kuona watendaji wanakua kikwazo katika kufanikisha mpango huo na kwamba hatawavumilia.

" wakati Serikali ikijenga mazingira rafiki na wawekezaji sisi wenyewe mafisa wa Serikali tumekuwa kikwazo ,   Nae Meneja wa kampuni  GF Vehcle Assemblers , Ezra Mereng alisema lengo  lao ni kuunda kila aina ya chapa (brand ) ya magari kwa kuwa teknolojia na mitambo waliyonayo inauwezo wa kuunganisha magari aina zote zenye viwango na vigezo vya kitaifa na kimataifa.

 Mereng alisema kiwanda hicho kilianza kwa kuunda magari chapa aina ya FAW na sasa  wamezindua  chapa ingine  ya Hongyan  na kuwataka wadau na makampuni mengine  ya magari kuacha kuagiza badala yake walete GFA kuundiwa (Assembling) kwa zingatia vigezo vyoote vya kimataifa.

Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge akikata utepe kuashiria uzinduzi wa awamu ya pili ya utengenezaji wa gari mpya ya kubebea mizigo aina ya Hong Yang katika kiwanda cha GF  leo mkoani Pwani.
Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge  akipokea zawadi ya kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya GF Assemblers Imrani Karmali wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya utengenezaji wa gari jipya ya kubebea mizigo anina ya Hong Yang katika kiwanda hicho leo mkoani Pwani.
Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge akifurahia jambo na mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha GF Assemblers,Imrani Karmali  baada ya  uzinduzi wa awamu ya pili ya utengenezaji wa gari mpya ya kubebea mizigo aina ya  Hong Yan katika kiwanda hicho mkoani Pwani

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad