HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, February 10, 2021

ZAIDI YA WATU 8000 WANUFAIKA NA MIKOPO YA KILIMO

 

 Na Woinde Shizza , Michuzi Tv-Arusha


Zaidi ya wakulima 8000 wamenufaika na mikopo ya kilimo kutoka katika mradi wa mfuko wa dhamana kwa wakulima wadogo wadogo inayodhaminiwa na benki ya maendeleo ya kilimo (TADB) kwa  kushirikiana na taasisi nyingine za kifedha 10.

Akiongea na waandishi wa habari  Katika maonesho ya nne ya mifuko ya programu za uwezeshaji yanayoendelea mkoani Arusha  Afisa mwandamizi wa benki ya maendeleo ya kilimo George Nyamrunda, alisema kuwa mfuko huo ni mfuko unaoratibiwa na benki hiyo kwa ajili ya kuhamasisha au kuchagiza benki na taasisi nyingine za fedha ziweze kukopesha wakulima.

Alisema kuwa kwa muda mrefu wakulima wamekuwa wakikosa uwezeshaji kupitia  mabenki wakiambiwa kuwa hawakopesheki kwa sababu hawana dhamana  hivyo benki hiyo kupitia mfuko huo wamekuwaja na suluhu ya kuwapatia dhamana mabenki Ili waweze kukopesha wakulima.

“Mpaka sasa tuna ushirika na tasisi za kifedha kumi ambazo tunawapatia dhamana na wao waweze kuongeza uwekezaji katika kilimo ambapo kinachofanyika ni mabenki yanakopesha wakulima alafu benki ya kilimo inatoa dhamana na wakishindwa kulipa tunafidia ile hasara ambayo mabenki yamepata,” Alisema Nyamrunda.

Alieleza wameshadhamini mikopo ya zaidi  bilioni 69 kwa muda wa miaka miwili tangu kuanzishwa kea mfuko huo ambapo wameweza kuwafikia wanufaika 8500 huku asilimia 95 wakiwa ni wakulima wadogo.

Alifafanua kuwa lengo la mfuko huo ni kuhamasisha mabenki mengine kuisaidia benki ya kilimo ambayo ndio inajukumu la kuwezesha sekta ya kilimo lakini kutokana na uhitaji wa mitaji kikubwa wakahamasisha na mabenki mengine kuwekeza.

Aliendelea kusema kuwa faida kubwa waliyopata mpaka sasa ni kushusha ribya ya mikopo inayotolewa kwa wakulima kutoka Asilimia 20 hadi 24 na kufikia Asilimia 14 hadi 17.

Kwa upande wake Lucius Mtewele meneja mikopo ya kilimo kutoka benki ya TPB alisema kuwa wanategemea mashirikiano hayo Katika kuendeleza kilimo na wanaamini wataweza kuwafikia wakulima wengi zaidi na kunyanyua maisha yao.

Naye meneja mahusiano kilimo biashara  kutoka benki ya CRDB kanda ya kaskazini Rogers Mselle ushirikiano huo umeweza kuwasaidia kuwafulikia wakulima wengi zaidi na kuweza kuwafikia wakulima na kutoa mkopo zaidi ya bilioni 15 kupitia dhama iliyotolewa na benki ya maendeleo ya kilimo  na kufikia wanufaika 1200.
 Afisa mwandamizi wa benki ya maendeleo ya kilimo George Nyamrunda akiongea na waandishi wa habari katika maonesho ya nne ya mifuko ya programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi yanayofanyika Katika viwanja vya kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha

 Meneja mikopo ya kilimo kutoka benki ya TPB,Lucius Mtewele akiongea na waandishi wa habari katika maonesho hayo.
meneja mahusiano kilimo biashara  kutoka benki ya CRDB kanda ya kaskazini Rogers Mselle  akiongea na waandishi wa habari Katika maonesho ya nne ya mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi  yanayofanyika Katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.
 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad