Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Shaurimoyo, Senebius Mtega akizungumza na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni.
Mwalimu Mkuu Msaidizi Shule ya Msingi Maholong'wa, Bw. Chefasi Mdessa akizungumza ofisini kwake hivi karibuni.
Mwalimu
Mkuu Msaidizi Shule ya Msingi Matika, Ludan Njuu (kushoto), kulia ni
mmoja wa walimu maalum wa kujitolea wa darasa la jifunze shuleni hapo.
Na Joachim Mushi, Ludewa
BAADHI
ya walimu wakuu wa shule za msingi zinazotekeleza mradi wa majaribio wa
Darasa Jifunze ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, mkoani Njombe
wameomba mradi huo uwe endelevu ili kuwasaidia wanafunzi wanaokubwa na
changamoto ya ujifunzani hadi kufika darasa la tatu na kuendelea wakiwa
hawajui kusoma na kuandika.
Kauli
hiyo imetolewa hivi karibuni wilayani Ludewa kwa nyakati tofauti na
walimu hao katika mahojiano na mwandishi wa habari hizi kuzungumzia
maendeleo ya mradi wa darasa jifunze uliokuwa ukitekelezwa kwenye shule
zao.
Mwalimu
Mkuu Msaidizi Shule ya Msingi Maholong'wa, Bw. Chefasi Mdessa
akizungumza amesema kuna mafanikio makubwa ya mradi huo unaotekelezwa
kwa majaribio katika shule hiyo, jambo ambalo limeleta matumaini kwao na
hivyo kushauri ikiwezekana mradi huo uendelee kutekelezwa katika shule
za msingi zenye changamoto ya ujifunzaji.
Alisema
tathimini iliyofanywa kubaini wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika
kuanzia darasa la kwanza hadi la sita katika shule hiyo, ilibainini
wanafunzi 83 wakiwa hawajui kusoma vizuri na hivyo kuingizwa rasmi
katika mradi wa Jifunze uliotekelezwa kwa awamu tatu zenye siku 10.
Alisema ndani ya siku 30 za utekelezaji mradi huo ilifanikisha
kuwawezesha idadi kubwa ya wanafunzi na kusalia 9 tu ambao walikuwa bado
na changamoto hiyo.
"...Mapendekezo
mengine binafsi natamani mradi huu uwe wa kudumu shuleni hapa na
utumike kwa kufundishia darasa la awali, darasa la kwanza na kwa darasa
la pili, naamini mafanikio tulioyapata kwa muda mfupi tukiingiza mfumo
huu ukawa wa kudumu tutapunguza kwa kiasi kikubwa wanafunzi waliojua
kusoma na kuandika katika shule zetu," alisema Bw. Chefasi Mdessa.
Kwa
upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Shaurimoyo, Senebius Mtega
alisema mradi wa darasa la Jifunze ulianza kutekelezwa katika shule
hiyo tangu mwezi Agosti 2020 ukiwa na wanafunzi 78 wasiojua kusoma na
kuandika katika hatua mbalimbali ulikuwa na mafanikio makubwa ndani ya
kipindi kifupi. Alisema wapo wanafunzi ambao walikuwa wanashindwa kusoma
herufi, wengine pia kushindwa kusoma maneno na pia wapo ambao
walishindwa kusoma aya; ambapo waligawanywa kulingana na changamoto zao
za ujifunzaji lakini idadi kubwa ilifanikiwa.
"...Tulianza
kutekeleza mradi tukiwa na wanafunzi 78, kimsingi mradi huu umetusaidia
sana kwani wanafunzi wengi wamefaulu kutoka katika changamoto ya awali
ya kutokumudu kusoma na kuandika kwa ufasaha. Ni mradi mzuri tunaupenda
na tunapenda hata uwe endelevu hapa kwetu na hata kwenye shule zingine,"
aliongeza Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Shaurimoyo, Bw. Mtega.
Naye
Mwalimu Mkuu Msaidizi Shule ya Msingi Matika, Ludan Njuu anasema hadi
wanaanza kutekeleza mradi wa Jifunze walikuwa na jumla ya wanafunzi 75,
waliokuwa na changamoto za usomaji kwenye madaraja ya aya, maneno na
silabi, lakini hadi mwisho wa mradi zinakamilika siku 30 ni wanafunzi 13
pekee ndio walikuwa na changamoto hiyo, huku wengine wote wakifanikiwa
kuvuka katika changamoto hiyo.
"...Kimsingi
zoezi hili kama litaendelea watoto wengi walio na changamoto hiyo
tunaweza kuwapunguza. Alishauri viongozi sekta ya elimu kwa kushirikiana
na Uwezo Tanzania kuangalia namna ya kuufanya mradi huo uwe endelevu na
kutekelezwa shule zote kwa madarasa ya awali, darasa la kwanza na la
pili ili kumaliza kabisha changamoto hiyo ambayo ipo katika maeneo
kadhaa," alisema mwalimu huyo.
No comments:
Post a Comment