Katika
kuhitimisha Mwezi wa Huduma kwa Wateja, Benki ya NMB, imewakutanisha na
kuwapa watoto zaidi ya 25 elimu kuhusu masuala ya kuweka akiba na
nidhamu ya fedha.
Akizungumza
wakati wa utoaji elimu huo, ulioambatana na ufunguaji wa akaunti
mbalimbali zilizo chini ya mwamvuli wa WAJIBU, Meneja wa NMB Tawi la
Oyster Plaza - Hildegard Mung'ong'o, alisema elimu waliyopewa watoto hao
ililenga kuwajengea utamaduni endelevu wa kuweka akiba tangu wakiwa
wadogo.
Meneja
wa NMB Tawi la Oyster Plaza - Hildegard Mung'ong'o akiangalia jinsi
mtoto Myreen Rashid akiweka pesa ikiwa ni sehemu ya kujifunza kuhusu
kuweka tangu wakiwa watoto.
Hildergard
alibainisha kuwa, Tawi lake pamoja na matawi yote ya NMB nchini huwa
yanajisikia Furaha kukutana na watoto pamoja na wazazi kuwapa elimu juu
ya masuala ya kifedha (WAJIBU) inayojumuisha akaunti tatu za Mtoto
Akaunti, Chipukizi Akaunti na Mwanachuo Akaunti.
Watoto wakiwa katika Tawi la Benki ya NMB Oyster Plaza wakipata elimu ya fedha.
Kwa
upande wake, Meneja Miradi wa Masula ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR),
Lilian Kisamba, alisema WAJIBU ni mwamvuli chanya katika ukuaji wa mtoto
kielimu na kinidhamu ya fedha, ulioanza tangu mwaka 2016.Tangu hapo,
WAJIBU kupitia akaunti za Mtoto, Chipukizi na Mwanachuo, umeweza
kuwafikia zaidi ya watoto 90,000 kote nchini.
Mameneja
hao waliwataka wazazi na walezi kujitokeza matawini kufungua akaunti za
watoto ambazo licha ya kadi ya Benki kuwa nayo mtoto, mzazi atabaki
kuwa msimamizi mkuu wa akaunti kwa kutambua miamala inayofanyika.
NMB
kupitia WAJIBU, imelenga kuwa na taifa la kesho lenye uelewa wa kina wa
elimu ya masuala ya fedha, ndio maana ikaanzisha mpango maalumu
unaowajumuisha mzazi na mtoto, wakiamini wateja hujengwa tangu wakiwa
wadogo.
No comments:
Post a Comment