
Balozi
 wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Fatma Rajab alikutana na Shirika la 
Qatar Travel Mart (QTM) linalojishughulisha kutangaza utalii wa ndani na
 nje ya Qatar pamoja na kuandaa Maonesho ya Utalii. Shirika hilo 
linajiandaa kufanya Maonesho Makubwa ya Utalii yatakayofanyika tarehe 
17-19 November 2021. Mataifa mengi ya kigeni ya Asia, Ulaya na Marekani 
yanatarajiwa kushiriki Maonesho hayo pamoja na ofisi za Kibalozi ziliopo
 Qatar.
 Maonesho hayo yatatoa fursa kwa nchi kutangaza Biashara, uwekezaji na 
Sanaa. Mhe. Balozi amewaahidi kuwa Tanzania itashiriki kikamilifu kwenye
 Maonesho hayo. Aidha kabla ya Maonesho hayo Ubalozi utaandaa Mkutano wa
 Mtandao Webinar Conference mwezi Desemba 2020 baina ya Shirika hilo la 
QTM na TTB na ZTC ili kuelezea vivutio vya Utalii vya Tanzania na 
kukaribisha watalii kutoka Qatar
Wednesday, October 14, 2020
 
Tanzania Kutumia Maonesho Makubwa ya Qatar Kutangaza Utalii
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment