Marwa
Mwita Rubirya mkuu mpya wa mkoa wa Njombe akizungumza na viongozi mbali
mbali katika ofisi za mkoa wa Njombe mara baada ya kupokewa mkoani
humo.
Eng ,Marwa Mwita Rubirya mkuu mpya wa mkoa wa Njombe akiwasili katika ofisi za mkoa wa Njombe.
Eng, Marwa Mwita Rubirya mkuu mpya wa mkoa wa Njombe akisalimiana na baadhi ya viongozi mara baada ya kuwasili mkoani Njombe.
Na Amiri Kiligalila,Njombe
MKUU wa mkoa wa mpya wa Njombe Enjinia Marwa Mwita Rubirya
aliyeteuliwa na kuapishwa hivi karibuni na Rais John Pombe Magufuli ,
amewasili kituo cha kazi na kuzungumza na baadhi ya watumishi wa mkoa na
wilaya ya Njombe ambapo amesema atafanya ziara katika wilaya zote nne
za mkoa wa Njombe huku akiomba ushirikiano kwa viongozi wa wilaya hizo.
Mara baada ya kuwasili katika ofisi za mkoa, mkuu huyo mpya amepokea
taarifa kutoka kwa katibu tawala wa mkoa wa Njombe Bi,Catarina Revocat
na mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth Msafiri muda mfupi baada ya
kukaribishwa.
“Wananchi wa Njombe ni wananchi wasikivu,wachapakazi na tunaamini
utafanya nao kazi vizuri sana”. Alisema Catrina Revocat katibu tawala wa
mkoa wa Njombe
Eng.Marwa Mwita Rubirya ameahidi kushirikiana na viongozi wa
halmashauri mkoa na wilaya katika kutatua changamoto zinazowakabili
wananchi vijijini.
“Nitategemea ushirikiano mkubwa kwa wenzangu hapa na ambao wako
wilayani,najua taarifa itaandaliwa ili inisaidie kujifunza Njombe
tunafanya nini na ni wapi tuongeze nguvu zaidi ili hatimaye tuwasaidie
wananchi”alisema Eng.Marwa Mwita Rubirya
Rubirya awali alikuwa meneja wakala wa barabara Tanzania (TANROD)
mkoa wa Mwanza na amechukuwa nafasi ya aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Njombe
Cristopher Ole Sendeka aliyekwenda kwenye majukumu mengine ya kisiasa.
No comments:
Post a Comment