HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 6, 2019

27 WAITWA TAIFA STARS, KUKIPIGA NA EQUATORIAL GUINEA NOVEMBA 15

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

KOCHA Mkuu wa Timu ya Tanzania 'Taifa Stars' Etienne Ndayiragije ameteua kikosi cha wachezaji 27 kitakachochea mcheo wa kwanza wa kufuzu mataifa Afrika (AFCON) 2021.

Ndayiragije ametangaa kikosi hico leo kitachoingia kambini mwishoni mwa wiki kujiandaa na mchezo wa kwanza dhidi ya Equatorial Guinea Novemba 15 utakaochezwa katika dimba la Uwanja wa Taifa.

Kikosi hicho kitawajumisha na wachezaji wanaocheza soka la kulipwa nje ya Tanzania akiwemo Mshambuliaji wa Genk Mbwana Samatta, Mshambuliaji wa Difaa El Jadida ya nchini Morocco Simon Msuva, Kiungo wa Tenerrife ya Hispania Farid Mussa. Beki wa Kulia wa Nkana ya nchini Zambia Hassan Kessy , David Kisu (Gor Mahia )na Eliuter Mpepo kutoka Buildcon Zambia.

Wachezaji wengine ni Magolikpa Juma Kaseja (KMC), Metacha Mnata (Yanga) na mabeki ni Salum Kimenya (TZ Prisons), Mohamed Hussein (Simba), Gadriel Michael (Simba), Erasto Nyoni (Simba)Bakari Nondo (Coastal Union), Kelvin Yondani (Yanga), Dickson Job (Mtibwa).

Viungo ni Jonas Mkude (Simba), Abdul Aziz Makame (Yanga), Iddi Suleimani (Azam), Salum Abubakar (Azam),  Mzamiru Yassin (Simba), Frank Domayo (Azam), Miraji Athuman (Simba), Hassan Dilunga (Simba).

Kwa upande wa safu ya usambuliaji wenine ni Ditram Nchimbi (Polisi TZ), Shaban Iddi (Azam),Kelvin John ( Football House) na Ayoub Lyanga (Coastal Union).

Taifa Stars ina kibarua cha kuhakikisha wanapata ushindi kwenye mchezo huo wa kwanza ili kuanza kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kwenda AFCON 2021.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad