HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 17, 2019

Abdallah Hussein awabeba Watanzania kwenye Pool Afrika Mashariki

Mkurugenzi wa Cuespory Maaters Limited, James Nderitu Kuria (kulia) Akimkabidhi Amos Ndyagumanawe pesa taslimu shilingi 50,000 ya Kenya sawa na 1,000,000/= ya Tanzania mara baada ya kuibuka bingwa kwenye mashindano ya pool yajulikanayo kama "East Africa Chinise 8 Ball Competitions 2019" yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Moran Lounge & Grill Nanyuki nchini Kenya.
Bingwa wa Mashindano ya Pool yajjulikanayo kama "East Africa Chinise 8 Ball Competitions 2019" , Amos Ndyagumanawe kutoka Uganda akishangilia na kikombe pamoja na pesa taslimu shilingi 50,000 ya Kenya sawa na 1,000 000/= ya Tanzania yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Moran Lounge and Grill Nanyuki nchini Kenya.
Mkurugenzi wa Cuespory Maaters Limited, James Nderitu Kuria (kulia) Akimkabidhi Abdallah Hussein pesa taslimu shilingi 5,000 ya Kenya sawa na 100,000/= ya Tanzania mara baada ya kushinda kuingia robo fainali ya mashindano ya Pool yaliyojulikana kwa "East Africa Chinise 8 Ball Competitions 2019" yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Moran Lounge & Grill Nanyuki nchini Kenya. 

MCHEZAJI wa Pooltable, Abdallah Hissein(Sniper) amewabeba Watanzania kwa kutinga robo fainali  ya mchezaji mmoja mmoja(Singles) katika fainali za mashindano ya East Afrika ya mchezo huo yaliyojulikana kwa "East Africa Chinise 8 Ball Competitions 2019" yaliyo malizika mwishoni mwa wiki Nanyuki nchini Kenya.

Mashindano hayo yalijumuisha wachezaji kutoka Nchi tatu ikiwani Tanzania, Uganda na Tanzania kwa siku mbili ambapo yalifungukiwa rasmi octoba 12 hadi 13,2019 yakikutanisha jumla ya wachezaji 64 kwa udhamini wa Moran Lounge & Grill.

Bingwa alieibuka katika mashindano hayo ni Amos Ndyagumanawe kutoka nchini Uganda ambapo alizawadiwa shingi 50,000 ya Kenya sawa na 1,000 000/= ya Tanzania.
Msindi wa pili ni John Kyalo kutoka Kenya ambaye alizawadiwa shilingi 30,000 ya Kenya sawa na 600,000/= ya Tanzania, mshindi wa tatu ni Dennis Kimani kutoka Kenya ambaye alizawadiwa shilingi 20,000 ya Kenya sawa na shilingi 400,000/= ya Tanzanian na mshindi wa nne ni Collins Tuwei kotoka Kenya ambaye alizawadiwa pesa taslimu shilingi 10,000 ya Kenya sawa na 200,000/= ya Tanzania na wasindi wengine walioingia nane bora ni Abdallah Hussein kutoka Tanzania, Henry Mwangi kutoka Kenya, David Njane kutoka Kenya na Martin Mwangi kutoka Kenya ambao walizawadiwa shilingi 5,000 ya Kenya kila mmoja sawa na 100,000/= ya Tanzania.

Akizungumza na Wanahabari,Wachezaji pamoja na wadai waliojitokeza kushuhudia mashindano hayo, Mkurugenzi wa Cresports Masters Limited
James Nderitu Kuria kwanza aliwapongeza wachezaji kutoka nchi mbalimbali kuja kuungana na wenyeji Kenya kwenye mashindano hayo na kuwaomba sasa ni wakati wa kujikita kuwekeza katika mchezaji mmoja mmoja na si team.

Alisema Kuria kuwa alifurahiswa sana na mwitikio wa wachezaji wengi waliojitokeza na kuahidi mashindano haya leo yamefanyika Kenya awamu ijayo yatakuwa nchi nyingine ili kuleta hamasa zaidi.

Mwisho alimpongeza bingwa Amos Ndyagumanawe kwa kufanikiwa kupata ubingwa huo 2019 kwani kwa uwezo aliouonyesha hakika alistaili kuwa bingwa na pengine maandalizi aliyoyafanya.Lakini pia aliwapongeza washindi wengine wote na kuwaomba wakafanye mazoezi kwa maandalizi ya mashindano yajayo ambayo watatangaziwa.

Nae mratibu wa Mkurugenzi wa Athletes Committee (ICEA) ,Peter Gichuhi Kinyua aliwapongeza wachezaji wote na wadau wa Chinise 8 Ball kwa kujitokeza kushiriki na kuwapongeza walifanikiwa kushinda na kuwaomba walioshindwa wakajipange kwa mashindano yajayo.

Katika Mashindano hayo ya Chinise 8 Ball yaliwakilishwa na wachezaji wanne kwa udhamini wa Kampuni ya kutengeneza meza za Pool ya Kenice ambao ni Abdallah Hussein(Dar), Baraka Jackson(Manyara), Amos Bonophace (Dar) na Michael Machellah(Dar).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad